HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, January 24, 2015

demo-image

KAMERA YA MTAA KWA MTAA NA TASWIRA MBALI MBALI KUTOKA MAHAKAMA YA NDIZI,MABIBO JIJINI DAR

DSC_0440
Kamera ya Mtaa kwa Mtaa Blog,leo hii ilipata wasaa wa kukatiza kwenye Soko la Ndizi Mabibo (maarufu kama Mahakama ya ndizi) jijini Dar es salaam na kufanikiwa kunasa taswira mbalimbali katika soko hilo maarufu hapa jijini Dar.Soka hili linasifika sana kwa kuwa na ndizi za kila aina nyingi na zinazotoka katika mikoa ya Mbeya,Kilimanjaro na Kagera.Pichani ni mmoja wa wauzaji wa ndizi hizo akiwa amebeba mkungu kuutoa sehemu moja kwenda nyingine.
DSC_0448
Ndizi aina ya Mshale zilisubiri kushushwa kutoka kwenye lori lililokuwepo sokoni hapo.
DSC_0453
DSC_0455
Wafanyabiashara wa soko hili,muda wote wako bize,kwani wateja hawakatiki sokoni hapo hasa siku za mapumziko ya wiki kama leo.
DSC_0457
Ndizi zikipakiwa kwenye Mkokoteni.
DSC_0462
Mandhali tulivu ya soko hilo kama ilivyonaswa na Kamera ya Mtaa kwa Mtaa leo.
DSC_0470
Mzee wa kubeba dabo dabo akiwahisha ndizi kwa mteja.
DSC_0472
"......hizi zote bei gani?...." Wanaonekana Wateja hao wakimuuliza muuzaji.
DSC_0499
Hizi nazo zimevundikwa kwa utaalamu wa kuzivunika kwa majani ya mgomba.
DSC_0502
Maparachichi nayo yanapatikana kwenye shoko hili la Mahakama ya ndizi.
DSC_0505
Mapasheni pia ndani.
DSC_0508
Mananasi ndio usiseme,maana ni kama uzao wake unaendana na ndizi hizo.
DSC_0421
Viazi ulaya.
DSC_0516
DSC_0518
Mzigo mwingine ukiendelea kushuka.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Contact Form

Name

Email *

Message *