HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, December 6, 2016

LIGI KUU VODACOM KUTIMUA VUMBI DESEMBA 17, SIMBA NA YANGA FEBRUARI 18

Ofisa habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF) Alfred Lucas


Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
LIGI kuu Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea tena kwa duru la pili kuanzia Desemnba 17, huku timu zikishauriwa kukamilisha usajili kwa wakati huku Yanga na Simba kuumana Februari 18 2017..

Dirisha la usajili lililofunguliwa Novemba 15 linatarajiwa kufungwa Desemba 15 na timu zote zimeopewa mwongozo wa kutumia mfumo wa ule ule wa kutumia mtandao katika kuwasilisha majina hayo usiku wa Desemba 15.

Ofisa habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF) Alfred Lucas amesema kuwa ligi inatarajiwa kuanza Desemba 17 kwa mechi nne kuchezwa kwenye viwanja tofauti nchini.

Lucas amesema kuwa kwa sasa ratiba hii imezingatia kalenda ya michezo ya kimataifa, kombe la mapinduzi na kombe la Shirikisho ilihali hawajaweza kuweka ratiba ya michezo ya kimataifa kwa timu zinazoshiriki michuano hiyo kwani ratiba ya Shirikisho la Mpira Afrika bado hawajaweka raiba wazi.

Katika ratiba hiyo, Kikosi cha Simba kitaanzia ugenini kuvaana Ndanda huku mabingwa watetezi Yanga wakiwa Uwanja wa Taifa kuumana na JKT Ruvu na Azam watakuwa ugeninio dhidi ya African Lyon.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad