HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, November 3, 2016

UNESCO YAKEMEA SHERIA ZINAZOKANDAMIZA UHURU WA HABARI


Mkuu wa idara ya mawasiliano na habari wa UNESCO, Ofisi za Tanzania, Christophe Legay akizungumza machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kufungua kongamano linalohusu ukatili kwa waandishi ikiwa ni maadhimisho ya siku ya kupinga ukatili kimataifa kwa waandishi wa habari, lililofanyika jana jijini Dar es Salaam. (Picha na Habari na Zainul Mzige wa Modewjiblog)

WAKATI Bunge la Tanzania wiki hii linatarajiwa kujadili na kupitisha muswada wa habari, Shirika la Umoja wa mataifa la Elimu, sayansi na Utamaduni (UNESCO) limehadharisha juu ya uwapo wa sheria zinazotishia uhuru wa vyombo vya habari.

Akizungumza katika kongamano linalohusu ukatili kwa waandishi ikiwa ni maadhimisho ya siku ya kupinga ukatili kimataifa kwa waandishi wa habari, Mkuu wa idara ya mawasiliano na habari wa UNESCO, Ofisi za Tanzania, Christophe Legay alisema katika utekelezaji wa maendeleo endelevu sekta ya habari ni muhimu na hivyo watendaji wake wanatakiwa kuwekewa mazingira huru ya kiutendaji.

Serikali ya Tanzania imepeleka muswada wa habari ambao unalalamikiwa na wadau wa habari kwamba haukupatiwa muda wa kutosha wa kujadiliwa na kuondolewa kwa vipengele ambavyo vinawanyima waandishi wa habari uwezo wa kuandika.
Aidha ndani ya muswada huo imeelezwa na Jukwaa la Wahariri kwamba kuna vipengele ambavyo vinakwamisha umahiri wa uandishi na uchunguzi kama kufutiwa kwa leseni na kuuzwa kwa mitambo kutokana na makosa mbalimbali ambayo yamegeuzwa ya jinai.

Aidha wadau hao wanasema kwamba serikali imejitengenezea nafasi ya kuwa na nguvu kubwa ya kudhibiti habari kupitia Kurugenzi ya Maelezo na Waziri mwenyewe huku Bodi iliyopangwa kuwa huru ikionekana kwamba haina nguvu zakutosha.

Akizungumza haja ya mazingira rafiki Legay alisisitiza kuwaTaifa linastahili kuhakikisha kwamba kumewekwa mazingira rafiki ya upatikanaji wa habari na kwamba kila mwananchi anapata haki yake ya kupata, kusambaza habari kwa mujibu wa mikataba ya kimataifa na sheria zinazohusu habari za taifa.

Kaimu Mkurugenzi Idara ya Habari Maelezo, Jamal Zuberi akizungumza akifungua kongamano linalohusu ukatili kwa waandishi ikiwa ni maadhimisho ya siku ya kupinga ukatili kimataifa kwa waandishi wa habari kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Elisante Ole Gabriel, lililofanyika jana jijini Dar es Salaam.

Alisema ingawa haki ya kupata habari imeelezwa waziwazi katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia vifungu 18 na 21 mambo yanayojitokeza sasa katika sheria za habari nchini Tanzania yanatishia haki hiyo, kutokana na sheria hizo kuonekana kubana uchakataji wa habari. Akitolea mfano wa sheria ya huduma ya habari ya mwaka 2016.

Alisema katika mkakati wa utekelezaji wa malengo endelevu ya dunia kuna mpango mkakati wa kulinda waandishi wa habari na upatikanaji wa habari kama ilivyoelezwa katika lengo namba 16, kifungu kidogo cha 10.

Alisema kwa sasa dunia inakabiliwa na tishio kubwa la upatikanaji wa habari kutokana na vitisho vinavyowekwa kwa waandishi wa habari ikiwa na pamoja na kuuawa, kutiwa kizuini au kupotea bila kujulikana.

Alisema katika muongo mmoja uliopita waandishi 827 waliuawa na kwamba ni asilimia 7 tu ya mauaji hayo yalipatiwa ufumbuzi. Aidha alisema mwaka jana ulikuwa mwaka mbaya zaidi kwa waandishi wa habari, huku waandishi 16 pekee wakiuawa katika bara la Afrika.

Mkurugenzi wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), Onesmo Olengurumwa akijadili rasimu ya mkakati wa mpango wa usalama wa waandishi wa habari wakati wa kongamano linalohusu ukatili kwa waandishi ikiwa ni maadhimisho ya siku ya kupinga ukatili kimataifa, lililofanyika jana jijini Dar es Salaam.

Alisema kitendo cha kuwadhibiti waandishi wa habari kunaashiria udhibiti wa upatikanaji wa habari huru ambao ndio msingi wa demokrasia na maendeleo ya jamii.

Aliitaka jamii kuhakikisha kwamba inakaa pamoja na kuona haja ya kulinda uhuru wa habari ikiwa na pamoja na kuwalinda wachakataji habari ili kila mtu anayetaka kupata habari aweze kuipata na kuitumia kwa maendeleo yake, jamii na taifa.

Akimkariri Mkurugenzi Mkuu wa Unesco Irina Bokova, mkuu huyo wa mawasiliano alisema kwamba ukatili na vitendo vinavyoshabihiana navyo dhidi ya waandishi wa habari ni kinyume na uhuru na haki ya upatikanaji wa habari na wanaofanya mambo hayo wanatishia utawala bora wa kisheria na kusababisha utoaji habari usiokamili kwa hofu ya udhibiti na matokeo yake jamii nzima inapotoka na kuhangaika. Leo hii tunahitaji dhamira mpya ya kuhakikisha kwamba tunatengeneza mazingira salama na rafiki kwa waandishi wa habari.

UNESCO ni mdau mkubwa wa habari nchini Tanzania na katika taarifa yake kwa vyombo vya habari ilikumbushia kazi inayofanya pamoja na wadau wengine wa habari wakiongozwa na Tanzania Human Rights Defenders Coalition kutengeneza mpango kazi wa ushawishi wa namna bora ya kuchakata na kufanyakazi ya uandishi wa habari nchini Tanzania.
Mdau wa tasnia ya habari, Kenneth Simbaya akiwasilisha fursa na changamoto walizokumbana nazo wakati wa uandaaji wa rasimu ya mkakati wa mpango wa usalama wa waandishi wa habari katika kongamano linalohusu ukatili kwa waandishi ikiwa ni maadhimisho ya siku ya kupinga ukatili kimataifa, lililofanyika jana jijini Dar es Salaam.

Kutokana na mkakati huo mwaka jana kuliundwa kikosi kazi cha kuangalia usalama wa waandishi wa habari na taarifa inatarajiwa kutolewa wakati wowote kuanzia sasa namna bora ya kuwawezesha waandishi wa habari kufanyakazi kwa usalama.

Naye msemaji wa serikali ya Tanzania akizungumza Kaimu Mkurugenzi Idara ya Habari Maelezo, Jamal Zuberi akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Elisante Ole Gabriel katika tukio hilo alitoa wito kwa taasisi zisizo za kiserikali, taasisi za sheria na vyombo vya habari kuhakikisha kwamba mazingira ya kufanyia kazi waandishi wa habari ni salama na haki za upatikanaji wa habari haudhibitiwi.

Alisema ili kuwezesha hali hiyo serikali imepeleka muswada wa waandishi wa habari bungeni na pia ikiwa kama moja ya nchi iliotia saini mikataba ya kimataifa kuhusu upatikanaji wa habari serikali itafanyakazi kwa pamoja na wadau kuhakikisha kwamba waandishi wa habari wanapata mazingira rafiki na salama ya kufanyia kazi.
Mmoja wadau wa masuala ya sheria akizungumza jambo katika kongamano linalohusu ukatili kwa waandishi ikiwa ni maadhimisho ya siku ya kupinga ukatili kimataifa kwa waandishi wa habari, lililofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Mwanasheria kutoka Nola, James Marenga akifafanua jambo wakati wa kongamano linalohusu ukatili kwa waandishi ikiwa ni maadhimisho ya siku ya kupinga ukatili kimataifa kwa waandishi wa habari, lililofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi Idara ya Habari Maelezo, Jamal Zuberi (kushoto) akiwa na wadau wa tasnia ya habari wakati wa kongamano linalohusu ukatili kwa waandishi ikiwa ni maadhimisho ya siku ya kupinga ukatili kimataifa kwa waandishi wa habari, lililofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Wadau wa tasnia ya habari na masuala ya Sheria walioshiriki kwenye kongamano linalohusu ukatili kwa waandishi ikiwa ni maadhimisho ya siku ya kupinga ukatili kimataifa kwa waandishi wa habari, lililofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Washiriki wakitazama moja ya video ya shuhuda inayozungumzia usalama wa waandishi wa habari wakati wa uchaguzi wakati wa kongamano linalohusu ukatili kwa waandishi ikiwa ni maadhimisho ya siku ya kupinga ukatili kimataifa, lililofanyika jana jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad