Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh.Amos Makalla watano kutoka kushoto akiwa katika picha ya pamoja na Vijana walio hitimu Mafunzo ya ujasiriamali kwa Vijana 1,811 kutoka jiji la Mbeya na Wilaya ya Rungwe Mafunzo yaliyo ratifies na shirika la Techoserve,
Mkuu wa mkoa wa mbeya Amos Makalla amewaagiza wakurugenzi wa Halmashauri zote Mkoa wa Mbeya kutenga maeneo kwa ajili ya wajasiriamali wakiwemo Vijana ili wafanye biashara na viwanda vidogo vidogo
Hayo ameyasema wakati akifunga Mafunzo ya ujasiriamali kwa Vijana 1,811 kutoka jiji la Mbeya na Wilaya YA Rungwe Mafunzo yaliyo ratifies na shirika la Techoserve
Aidha Amewataka kutenga Fedha kupitia mapato YA ndani na kutoa mikopo nafuu kwa Vijana na wanawake kwa kufanya hivyo itasaidia Makundi hayo kuanzisha au kukuza biashara zao,
Pia Amewataka Vijana kutobweteka badala yake wajishughulishe na kutumia fursa zilizopo ktk jamii kujipatia kipato.
Amesema hakuna serikali itakayokuja na kuwafuata vijiweni ili iwapatie Fedha bali atahahakikisha maeneo YA kufanyia biashara au kilimo wanawapatia Vijana wenye kuhitaji na sambamba na hilo Halmashauri zitenge Fedha kwa ajili ya mikopo YA riba nafuu.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh.Amos Makalla akizungumza na Wahitimu wa Mafunzo Ya Ujasiliamali yaliyofanyika katika ukumbi wa Tughimbe Mafiati Jijini Mbeya.
Baadhi ya Wahitimu wa Mafunzo ya ujasiliamali wakiwa ndani ya ukumbi wa Tughimbe Kusikiliza na Kusherehekea Hafra hiyo ya Uhitimu wa Mafunzo ya ujasiliamali.
No comments:
Post a Comment