HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, November 6, 2016

KAMA ULIPITWA NA MECHI YA SIMBA NA AFRICAN LYON LEO, BASI PICHA HIZI ZITAKUFAA KABISA

 
Mshambuliaji wa Timu ya African Lyon, Omary Abdallah akiwatoka mabeki wa Timu ya Simba, Novality LUfunga na Jonas Mkude, katika Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, uliochezwa jioni ya leo katika Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es salaam. African Lyon imeshinda bao 1-0.
 
Timu ya African Lyon imefanikiwa kuondoka na alama tatu katika Uwanja wa Uhuru baada ya kuifunga Simba goli dakika ya 96 na kuweka rekodi ya kuwafunga wekundu hao wa Msimbazi toka ligi ianze.

African Lyon waliweza kucheza kwa makini na waliweza kutumiawaliitumia kwenye kipindi cha kwanza, ilizaa matunda kutokana na kuibana Simba ambayo ilionekana kushindwa kabisa kupenya safu ya ulinzi ya Lyon.

Pamoja na kujitahidi kutengeneza nafasi za mabao na kupata kona tatu kwenye kipindi cha kwanza, mashambulizi mengi ya Simba yaliishia mikononi mwa kipa Youthe Rostand wa Lyon ambaye alikuwa kikwazo kwenye mchezo huo.

Dakika nne za nyongeza kwenye mchezo huo, zilikuwa chungu kwa Simba baada ya mshambuliaji Abdallah Msuhi kuitumia vyema krosi Ya Rahidhan Hafidh na kuifungia bao Lyon ambalo limevunja rekodi ya Simba kucheza mechi 13 za ligi bila kupoteza.

Kufungwa kwa bao hilo kuliwachochea mashabiki wa Simba ambao walianza kurusha makopo ya maji uwanjani wakionyesha kutoridhishwa na mwamuzi wa pembeni Frank Komba wakidai kuwa mpigaji wa krosi alikuwa ameotea. 
 Mshambuliaji wa Timu ya African Lyon, Abdullah Msuhi akiachia shuti lililoingia moja kwa moja wavuni na kuiandikia timu yake bao la kuongoza dhidi ya Timu ya Simba, katika Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, uliochezwa jioni ya leo katika Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es salaam. African Lyon imeshinda bao 1-0.
 Mshambuliaji wa Timu ya African Lyon, Abdullah Msuhi akiruka juu kushandilia goli lake dhidi ya Wekundu wa Msimbazi, katika Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, uliochezwa jioni ya leo katika Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es salaam. African Lyon imeshinda bao 1-0.
 
Mshambuliaji wa Simba, Laudit Mavugo akiichachafya ngome ya African Lyon. 
Kikosi cha Simba kilichoanza leo
Kikosi cha African Lyon.
Kipa wa Timu ya African Lyon, Rostand Youthe akiruka juu sambamba na Mshambuliaji wa Simba, Laudit Mavugo na kuudaka mpira kwa ustadi mkubwa.
Mshambuliaji Machachari wa Simba, Shiza Kichuya akiachia shuti kali kulekea langoni mwa Timu ya African Lyon ambalo lilienda moja kwa moja mikononi mwa mlinda mlango wa timu hiyo, Rostand Youthe.





 







Sehemu wa vingozi na wadau wa Timu ya Simba wakifatilia mtanange huo.
Mchezaji wa Simba, Fredrick Blagnan akiifatilia timu yake.















No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad