HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, November 8, 2016

Hospitali ya Kairuki yaboresha huduma zake

Hospitali ya Kairuki katika kuboresha huduma zake kwa wagonjwa imeanza kutumia kitengo kipya kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa wa kutwa  hususani wale wanachama wa mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).

Kitengo hicho kipya (OPD 3)  kilichopo nyuma ya Jengo kuu la hospital mkabala na kitengo cha magonjwa ya viungo (Physiotherapy Unit) kina sehemu kubwa ya mapokezi, vyumba  mbalimbali  vikiwemo  vyumba 10 via madaktari, maabara,Duma la dawa,sehemu ya sindano na kufunga vidonda,chumba cha ultrasound,mapokezi , huduma za chanjo ya watoto (RCH),chumba cha wauguzi na duka dogo la vinywaji na vitafunwa nk.

Kitengo hicho kipya kitaiwezesha hospitali hiyo kutoa huduma kwa haraka na ufanisi zaidi kwa wagonjwa wasiopungua 120,000 kwa mwaka hivyo kupunguza kero ya  foleni na msongamano iliokuwepo siku za nyuma.


Imetolewa na Afisa
Mahusiano, Arafa Mohamed
Wagonjwa wakisubiri kupata matibabu katika hospitali ya Kairuki.
Vyumba vya madaktari.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad