HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, October 6, 2016

WLAC WAZINDUA AWAMU YA TATU YA KAMPENI YA ‘TUNAWEZA’ JIJINI DAR

Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Dar es Salaam, Flora Masue (wa pili kulia) na Mkurugenzi wa Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake (WLAC), Theodosia Muholo (wa tatu kulia), wakikata utepe kuzindua rasmi Awamu ya Tatu ya Kampeni ya ‘Tunaweza’ wakati wa hafla ya uzinduzi huo uliofanyika leo kwenye Viwanja vya Biafra jijini Dar es Salaam. Kulia ni Jacckline Mlay wa Kitengo cha haki za Jinsia Oxfam na (kushoto) ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Kivulini ya jijini Mwanza, Yassin Ally.
Mgeni rasmi Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Dar es Salaam, Flora Masue (kulia) na Mkurugenzi wa Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake (WLAC), Theodosia Muholo (katikati), na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kivulini ya jijini Mwanza, Yassin Ally (wa pili kushoto) wakiinua Vipeperushi baada ya mgeni rasmi kuzindua Awamu ya Tatu ya Kampeni ya ‘Tunaweza’ wakati wa hafla ya uzinduzi huo uliofanyika leo kwenye Viwanja vya Biafra jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Dar es Salaam, Flora Masue (wa pili kulia) na Mkurugenzi wa Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake (WLAC), Theodosia Muholo (wa tatu kulia), na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kivulini ya jijini Mwanza, Yassin Ally (wa pili kushoto) Mkaguzi wa Polisi Prisca Komba wa Dawati la Jinsia Polisi Kinondoni (kushoto) na Jackline Mlay wa Kitengo cha haki za Jinsia Oxfam, kwa pamoja wakiinua vipeperushi baada ya mgeni rasmi kuzindua Awamu ya Tatu ya Kampeni ya ‘Tunaweza’ iliyofanyika kwenye Viwanja vya Biafra jijini Dar es Salaam, leo.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Mwacity Almas, akiimba na kucheza pamoja na baadhi ya kinamama waliohudhuria uzinduzi wa Awamu ya tatu ya Kampeni ya ‘Tunaweza’ ya Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake (WLAC), iliyozinduliwa leo kwenye Viwanja vya Biafra jijini Kinondoni, jijini Dar es Salaam. Picha na Mafoto Blog

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad