Na Shamimu Nyaki-WHUSM.
Katika kuhakikisha Watanzania wanafanya kazi kwa maendeleo yao na Taifa nchini Serikali imewataka wasanii mbalimbali kutumia Sanaa yao kuelimisha jamii umuhimu wa kufanya kazi kwa bidii.
Wito huo umetolewa jana Wilayani Bagamoyo na Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel katika hotuba yake ya kufunga Tamasha la 35 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo lililoandaliwa na Taasisi ya Sanaana Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa).
Katibu Mkuu katika hotuba yake iliyosomwa na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Sanaa ya Wizara hiyo Bibi. Leah Kihimbi amesema kuwa Wasanii wana nafasi kubwa ya kufikia Watanzania wengi kutokana na kazi zao hivyo watumie nafasi hiyo kutoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa Kufanya kazi.
“Wasanii mkidhamiria jambo hufanyika na uwezo wa kufanya hivyo mnao,ni vizuri mkatumia Sanaa yenu kuwaelimisha wanachi manufaa ya kufanya kazi kwao wenyewe na Taifa kwa ujumla”.Alisema Prof.Ole Gabriel.
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Dkt. Herbet Makoye mbali na kuwashukuru wasanii wote waliohudhuria Tamasha hilo amewataka pia waendelee kufanya Sanaa zenye ubora na zinazoitangaza Tanzania Ulimwenguni.
“Mmeshiriki vizuri katika Tamasha hili niwasihi muendelee kufanya Sanaa iliyo bora inayotangaza nchi yetu kote Ulimwenguni ukizingatia tunazo Sanaa za aina mbalimbali ikiwemo ngoma,muziki,filamu na sanaa za ufundi”.Aliongeza Dkt.Makoye.
Aidha msanii Ebeneza Lukas anaefanya muziki amesemaTamasha limempa ujuzi na weledi mkubwa katika Sanaa yake ukizingatia kuwa yeye ndio anaanza kufanya Sanaa.
Tamasha hilo lililofunguliwa Septemba 26 mwaka huu na Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa naMichezo Mhe.Anastazia Wambura limefungwa Oktoba mosi ambapo kazi mbalimbali za Sanaa zilifanyika ikiwa ni pamoja na makongamano na warsha mbalimbali.
Katika kuhakikisha Watanzania wanafanya kazi kwa maendeleo yao na Taifa nchini Serikali imewataka wasanii mbalimbali kutumia Sanaa yao kuelimisha jamii umuhimu wa kufanya kazi kwa bidii.
Wito huo umetolewa jana Wilayani Bagamoyo na Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel katika hotuba yake ya kufunga Tamasha la 35 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo lililoandaliwa na Taasisi ya Sanaana Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa).
Katibu Mkuu katika hotuba yake iliyosomwa na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Sanaa ya Wizara hiyo Bibi. Leah Kihimbi amesema kuwa Wasanii wana nafasi kubwa ya kufikia Watanzania wengi kutokana na kazi zao hivyo watumie nafasi hiyo kutoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa Kufanya kazi.
“Wasanii mkidhamiria jambo hufanyika na uwezo wa kufanya hivyo mnao,ni vizuri mkatumia Sanaa yenu kuwaelimisha wanachi manufaa ya kufanya kazi kwao wenyewe na Taifa kwa ujumla”.Alisema Prof.Ole Gabriel.
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Dkt. Herbet Makoye mbali na kuwashukuru wasanii wote waliohudhuria Tamasha hilo amewataka pia waendelee kufanya Sanaa zenye ubora na zinazoitangaza Tanzania Ulimwenguni.
“Mmeshiriki vizuri katika Tamasha hili niwasihi muendelee kufanya Sanaa iliyo bora inayotangaza nchi yetu kote Ulimwenguni ukizingatia tunazo Sanaa za aina mbalimbali ikiwemo ngoma,muziki,filamu na sanaa za ufundi”.Aliongeza Dkt.Makoye.
Aidha msanii Ebeneza Lukas anaefanya muziki amesemaTamasha limempa ujuzi na weledi mkubwa katika Sanaa yake ukizingatia kuwa yeye ndio anaanza kufanya Sanaa.
Tamasha hilo lililofunguliwa Septemba 26 mwaka huu na Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa naMichezo Mhe.Anastazia Wambura limefungwa Oktoba mosi ambapo kazi mbalimbali za Sanaa zilifanyika ikiwa ni pamoja na makongamano na warsha mbalimbali.
aimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Sanaa kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi Leah Kihimbi akizungumza na wahitimu pamoja na wageni mbalimbali (hawapo pichani) katika sherehe za mahafali ya 27 ya Chuo cha Ufundi na Sanaa Bagamoyo kilichopo chini ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Oktoba mosi Wilayani Bagamoyo.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo Dkt.Herbet Makoye akisoma hotuba kwa Mgeni Rasmi pamoja na wageni mbalimbali (hawapo pichani) katika sherehe za mahafali ya 27 ya Chuo cha Ufundi na Sanaa Bagamoyo kilichopo chini ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Oktoba mosi Wilayani Bagamoyo.
Mgeni rasmi ambaye ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Sanaa kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi Leah Kihimbi (wa tatu kulia) akiwatunuku vyeti vya kuhitimu Stashahada ya Sanaa na Ufundi baadhi ya wahitimu ) katika sherehe za mahafali ya 27 ya Chuo cha Ufundi na Sanaa Bagamoyo kilichopo chini ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Oktoba mosi Wilayani Bagamoyo.
Wanachuo wa Chuo cha Sanaa na Ufundi Bagamoyo wakicheza ngoma katika sherehe za mahafali ya 27 ya Chuo cha Ufundi na Sanaa Bagamoyo kilichopo chini ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Oktoba mosi Wilayani Bagamoyo.
Wahitimu wa ngazi ya Astashahada na Stashahada ya Sanaana Ufundi Bagamoyo wakicheza kwaya katika sherehe za mahafali ya 27 ya Chuo cha Ufundi na Sanaa Bagamoyo kilichopo chini ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Oktoba mosi Wilayani Bagamoyo.
Mgeni rasmi Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Sanaa kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi Leah Kihimbi (wa tatu kushoto waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) pamoja na wahitimu wa ngazi ya Astashaha katika sherehe za mahafali ya 27 ya Chuo cha Ufundi na Sanaa Bagamoyo kilichopo chini ya Taasisi hiyo .Wa kwanza Kulia Mkuu wa Idara ya Elimu ya Taasisi hiyo na Wa pili kulia ni Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo Dkt.Herbet Makoye.
Mgeni rasmi Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Sanaa kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi Leah Kihimbi (wa tatu kushoto waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) pamoja na wahitimu wa ngazi ya Stashaha katika sherehe za mahafali ya 27 ya Chuo cha Ufundi na Sanaa Bagamoyo kilichopo chini ya Taasisi hiyo .Wa kwanza Kulia Mkuu wa Idara ya Elimu ya Taasisi hiyo na Wa pili kulia ni Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo Dkt.Herbet Makoye.
Vikundi mbalimbali vya burudani kutoka Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) vikitoa burudani kwa wananchi pamoja na wasanii mbalimbali (hawapo pichani) katika ufungaji wa Tamasha la 35 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo lilioandaliwa na Taasisi hiyo Wilayani Bagamoyo Oktoba mosi.
Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Sanaa kutoka Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bibi Leah Kihimbi akiangalia bidhaa za urembo kutoka kwa mbunifu Mariam Kiiza kabla ya kufunga Tamasha la 35 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo lilioandaliwa na Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Wilayani Bagamoyo Oktoba mosi.
Baadhi ya wanachi walioshiriki ufungaji wa Tamasha la 35 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo lilioandaliwa na Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Wilayani Bagamoyo Oktoba mosi.
No comments:
Post a Comment