HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, October 14, 2016

LIGI KUU YA VODACOM TANZANIA BARA KUENDELEA KESHO, VIWANJA VITATU NYASI KUWAKA MOTO

Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) inatarajiwa kuendelea kesho Jumamosi Oktoba 15, 2016 kwa michezo mitatu ambako Simba inayoongoza katika msimamo wa kuwania taji hilo katika timu 16 itaikaribisha Kagera Sugar ya Kagera kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Katika mchezo huo Na.73, mwamuzi atakuwa Hussein Athuman kutoka mkoani Katavi ambako pembeni atasaidiwa na Joseph Bulali wa Tanga na Silvester Mwanga wa mkoani Kilimanjaro wakati Soud Lila wa Dar es Salaam atakuwa mwamuzi wa akiba huku Kamishna wa mchezo akiwa Pius Mashera wa Dodoma.

Mchezo mwingine utakuwa ni kati ya JKT Ruvu na Mwadui ya Shinyanga. Ni mchezo Na. 74 utakaofayika Uwanja wa Mabatini ulioko Mlandizi mkoani Pwani ambako utachezeshwa na Mwanamama mwamzi mwenye beji la FIFA, Mwanahamisi Matiku wa Dar es Salaam, akisaidiwa na Shafii Mohamed pia wa Dar es Salaam na Gesper Ketto wa Arusha.

Mwamuzi wa akiba atakuwa Abdallah Rashid wa Pwani wakati Kamishna wa mchezo huo atakuwa Charles Mchau wa Kilimanjaro.

Pia Stand United ya Shinyanya itaikaribisha African Lyon kwenye Uwanja wa CCM Kambarage katika mchezo Na. 75 ambao utachezeshwa na Eric Onoka wa Arusha akisaidiwa na Agnes Pantaleo pia wa Arusha na Omary Juma wa Dodoma wakati mwamuzi wa akiba atakuwa Joseph Pombe wa Shinyanga. Kamishna wa mchezo atakuwa Hamisi Kitila wa Singida.

Ligi hiyo itaendelea keshokutwa Jumapili kwa mchezo utakaozikutanisha timu za Azam na Young Africans; zote za Dar es Salaam. Mwamuzi wa mchezo huo Na. 76 atakuwa Israel Nkongo wa Dar es Salaam. Nkongo atasaidiwa na Soud Lila       na Frank Komba na mwamuzi wa akiba atakuwa Helen Mduma; wote wa Dar es Salaam. Kamishna wa mchezo atakuwa Michael Wambura pia wa Dar es Salaam.

Mchezo Na. 77 utazikutanisha timu za Ruvu Shooting na Mbeya City Jumapili Oktoba 16, 2016 kwenye Uwanja wa Mabatini mkoani Pwani. Mwamuzi wa mchezo huo atakuwa Rudovic Charles wa Tabora akisaidiwa na Samwel Mpenzu wa Arusha na Jeremina Simon    wa Dar es Salaam. Kamisha wa mchezo huo atakuwa Idelfonce Magali wa Morogoro.

Mtibwa Sugar ya Morogoro na Tanzania Prisons ya Mbeya nazo zitacheza Jumapili Oktoba 16 kwenye Uwanja wa Manungu mkoani Morogoro. Mchezo huo Na. 78 utachezeshwa na Elly Sasii wa Dar es Salaam. Waamuzi wasaidizi ni Ferdinand Chacha wa Mwanza Lulu Mushi wa Dar s Salaam wakati mwamuzi wa akiba Nicolaus Makalanga wa Morogoro. Kamishna ni George Komba wa Dodoma.

Kwa siku ya Jumapili mchezo mwingine utakuwa ni kati ya Toto African ya Majimaji ya Songea kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza. Mchezo huo Na. 79 utachezeshwa na mwamuzi Shomary Lawi wa Kagera akisaidiwa na Abdallah Uhako wa Arusha na Julius Kasitu wa Shinyanga huku mwamuzi wa akiba akiwa Mathew Akrama wa Mwanza. Kamishna atakuwa Michael Bundala wa Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad