Mkuu wa Zantel Zanzibar Mohamed Khamis Mussa-Baucha (Kulia) akisisitiza
jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu
uboreshwaji wa mtandao wa Zantel baada ya kuwasili vifaa vipya kutoka Ericsson
na Huawei Technologies. Akimsikiliza ni afisa wa Huawei William Cheng (Wei).
Mkuu wa Zantel Zanzibar Mohamed Khamis Mussa (kulia) akifurahia jambo na
maafisa waandamizi kutoka Zantel, Ericsson na Huawei, baada ya mkutano na
waandishi wa habari kuelezea mtandao ulioboreshwa wa Zantel unaoanza
kujengwa hivi karibuni. Mradi wa ujenzi huo unatarajiwa kukamilika ndani ya
miezi mitatu.
Alex Kamamia wa Ericsson (wa pili kulia) akielezea jinsi mtambo mpya wa
mawasiliano ya Zantel utakavyoboresha huduma kwa watumiaji wa mtandao wa
Zantel. Wakimsikiliza ni Mkuu wa Ufundi wa Zantel Larry Arthur (kushoto) na Jx
Chen wa Huawei (wa pili kushoto) na Frode Dyrdal (kulia) wa Ericsson.
Meneja Miradi wa Zantel Zanzibar Mohamed Ahmed Jaye, akielezea waandishi wa
habari (hawapo pichani), jinsi mitambo mipya ya Zantel inavyofanya kazi. Zantel
imeanza mradi mkubwa wa kuborersha mtandao wake nchi nzima kwa kufunga
mitambo mipya ya mawasiliano kwa ushirikiano na Huawei Technologies na
Ericsson.
Mkuu wa Ufundi wa Zantel Larry Arthur (wa pili kulia) akizungumza na waandishi
wa habari (hawapo pichani) kuhusu uboreshwaji wa mtandao wa Zantel baada ya
kuwasili vifaa vipya kutoka Ericsson na Huawei Technologies. Kushoto ni William
Cheng (Wei) kutoka Huawei, wa pili kushioto ni Mkuu wa Zantel Zanzibar,
Mohamed Khamis Mussa(Baucha), na kulia ni Frode Dyrdal wa Ericsson.
Mkuu wa Zantel Zanzibar Mohamed Khamis Mussa (wa pili kulia) na Mkuu wa
Ufundi wa Zantel Larry Arthur (wa pili kushoto), wakipongezana na wadau wao
wakubwa katika uboreshaji wa mtandao za Zantel unaotarajiwa kukamilika ndani
ya miezi mitatu ijayo. Kulia ni Frode Dyrdal wa Ericsson na kushoto ni William
Cheng wa Huawei.
Baadhi ya vifaa vipya vilivyowasili Zanzibar kutoka kampuni za Ericsson na Huawei
Technologies tayari kwa uboreshaji wa mtandao wa Zantel katika mradi wenye
gharama ya zaidi ya Tsh. 2bn/- unaotarajiwa kukamilika ndani ya miezi mitatu.
Baada ya kukamilika watuamiaji watapata mawasiliano yenye ubora zaidi.
No comments:
Post a Comment