HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, September 15, 2016

waliotekwa nyara Kongo watapatikana wakiwa salama - Serikali

Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi. Mindi Kasiga akizungumza na waandishi wa habari kuhusu juhudi zinazofanywa na Serikali katika kuwakoa watanzania waliotekwa nyara na waasi wa kikundi cha Maimai katika eneo la Namoyo jimbo la Kivu kusini katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii

Na. Immaculate Makilika- MAELEZO

Serikali imesema kuwa inashirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuhakikisha kuwa madereva wanaoendesha magari aina ya malori ambao wametekwa nyara jana na waasi wa kikundi cha Maimai katika eneo la Namoyo jimbo la Kivu kusini katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wanapatikana wakiwa salama.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi. Mindi Kasiga leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya juhudi zinazofanywa na Serikali katika kuwakoa watanzania waliotekwa nyara.

“Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Kongo inaendelea kufanya kila jitihada kuhakikisha madereva hao wanaachiwa huru haraka iwezekanavyo na kurudishwa nchini wakiwa salama”

“ Waasi hao wa Maimai wametoa masaa 24 hadi kufikia leo wawe wamelipwa kiasi cha Dola 4,000 kwa kila dereva ili waweze kuwaachia huru na kutishia kuwadhuru endapo hawatapata fedha hizo, hivyo basi Serikali imeendelea kuwa na mazungumzo na Serikali ya Kongo ili kupata ufumbuzi wa suala hili” alisema Kasiga

Aliongeza kuwa malori yaliyotekwa nyara ni 12 kati ya hayo nane ni mali ya mfanyabiashara wa kitanzania Bw. Azim Dewji na mengine ni mali za wafanyabiashara kutoka nchini Kenya.

Aidha, Serikali imewataka watanzania kufahamu hali ya usalama wa nchi wanazokwenda ili kujikinga na matatizo mbalimbali yanayoweza kuwapata wakiwa katika nchi hizo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad