HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, September 7, 2016

PICHA ZA MECHI YA SIMBA NA RUVU SHOOTING NIMEKUWEKEA HAPA, SIMBA YASHINDA BAO 2-1

Mshambuliaji wa Simba, Laudit Mavugo akiondoka na mpira katika mchezo wa Ligi kuu Tanzania Bara, dhidi ya Timu ya Ruvu Shooting, uliopogwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Uhuru, Jijini Dar es salaam. Simba imeshinda bao 2-1.
Winga machachari wa Timu ya Simba, Shiza Kichuya akijiandaa kuupiga mpira katika mchezo wa Ligi kuu Tanzania Bara, dhidi ya Timu ya Ruvu Shooting, uliopogwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Uhuru, Jijini Dar es salaam. Simba imeshinda bao 2-1.
Wazchezaji wa Timu ya Simba wakijipanga wakati wa Mpira wa adhabu ulioelekezwa langoni kwao.
Kiungo wa Simba, Said Ndemla akingalia namna ya kuondoka na mpira baada ya kuanguka na kuinuka, katika mchezo wa Ligi kuu Tanzania Bara, dhidi ya Timu ya Ruvu Shooting, uliopogwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Uhuru, Jijini Dar es salaam. Simba imeshinda bao 2-1.
Harakati ya kuwania mpira wa juu.
Mwinyi Kazimoto akiupokea mpira 
Ni heka heka ya kuwani mpira wa juu.
Kiungo wa Ruvu Shooting, Jabir Aziz akimkata ngwala Mshambuliaji wa Simba, Mzamiru Yassin wakati akiwa na mpira kulekea langoni kwao. Ngwala hiyo ilimpelekea Jabir Aziz kuzawadiwa Kadi nyekundu.
Mshabiki anapopandwa na mdadi pale amapoona mwamuzi hajaitendea haki timu yake.
Bambi kwa bambi, ni Shaaba Kisiga wa Ruvu Shooting na Beki wa Simba Novaty Lufunga.
Said Ndemla akiichambua ngome ya Ruvu Shooting.
Kikosi cha Ruvu JKT kilichoanza mchezo wa leo.
Kikosi cha Simba kilichoanza mchezo wa leo
Mwamuzi wa Mchezo, Ngole Mwangole akimzawadia kadi ya njano Mshambuliaji wa Timu ya Simba, Ibrahim Ajibu baada ya kujiangusha kwenye box la penati.
Wachezaji wa Ruvu Shooting wakishangilia baada ya kujipatia bao la kuongoza.
Mshambuliaji wa Timu ya Simba, Ibrahim Ajibu akishangilia baada ya kupatia timu yake bao la kusawazisha dhidi ya Ruvu Shooting.
Ni shangwe tupu.
Haondoki mtu na Mpira hapa.....
Mavugo wa Simba na Damas Makwaya wa Ruvu Shooting.
Washabiki wa Simba wakionyeshwa kukasirisha na jambo uwanjani.
Kiungo wa Ruvu Shooting, Jabir Aziz akiichachafya ngome ya Simba katika mchezo huo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad