Mgeni Rasmi, Bi. Lorah Madete, Kaimu Naibu Katibu Mtendaji, Klasta ya Uchumi Jumla,
Tume ya Mipango, akitoa hotuba wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku tano kuhusu
Usimamizi wa Uwekezaji wa Miradi ya Umma Kanda ya Morogoro kwa Maofisa na
Watendaji wa Idara za Sera na Mipango. Waliokaa ni Bi. Anna Kimwela, Mchumi, Tume
ya Mipango na Dr. Jehovaness Aikaeli, Mhadhiri Mwandamizi na Mkuu wa Idara ya
Uchumi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Washiriki wa Mafunzo kuhusu Mwongozo wa Usimamizi wa Uwekezaji wa Miradi ya
Umma ambao ni Maofisa na Watendaji wa Idara za Sera na Mipango kutoka Kanda ya
Morogoro wakimsikiliza Mgeni Rasmi (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mafunzo
hayo yanayofanyika katika Ukumbi wa Mkutano katika Chuo Kikuu cha Kilimo Morogroro
(SUA).
Muwezeshaji Dr. Jehovaness Aikaeli, Mhadhiri Mwandamizi na Mkuu wa Idara ya
Uchumi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akitoa elimu kwa washiriki wa mafunzo hayo.
Washiriki pamoja na wakufunzi wa mafunzo juu ya Mwongozo wa Usimamizi wa
Uwekezaji wa Miradi ya Umma ambao ni Maofisa na watendaji wa Idara za Sera na
Mipango kutoka Kanda ya Morogoro wakiwa katika picha ya pamoja na Mgeni Rasmi, Bi.
Lorah Madete, Kaimu Naibu Katibu Mtendaji, Klasta ya Uchumi Jumla, Tume ya
Mipango (aliyekaa wa pili kushoto) mara baada ya ufunguzi wa mafunzo hayo.
No comments:
Post a Comment