HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, September 30, 2016

MABONDIA KUPAMBANA OKTOBA 2 KIMARA KOROGWE, KUPIMA UZITO KESHO.

Na Mwandishi Wetu.
Mgeni rasmi katika 
mpambano wa Mabondia  mbalimbali watakaozipiga siku ya jumapili ya Oktober 2 katika ukumbi wa White House Bar Kimara Korogwe 
atakuwa  Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Humphrey Polepole. 

 Mambondia hao watapima uzito pamoja na Afya zao kesho jumamosi katika ukumbi wa White haouse kwa ajili ya kuzipiga siku inayo fuata.

akizungumzia mpambano uho kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini ambaye ni mratibu wa mpambano uho Rajabu Mhamila 'Super D' amesema kuwa mabondia wote watapia uzito pamoja na Faya Zao siku ya jumamosi.

aliwataja baadhi ya mabondia watakaozipiga na kesho watapima uzito ni Said Chino atakaezitwanga na haidar Mchanjo uzito wa kg 57 raundi sita wakati Abdallah Ruwanje atavaana na Shedrack Ignas mpambano wa raundi sita la uzito wa kg 63wakati bondia mkongwe kabisa katika mchezo wa masumbwi nchini Mustafa Doto atazipiga na bondia chipkizi Manyi Issa katika uzito wa kg 61 raundi sita.

mipambano mingine itawakutanisha mabondia Mohamed Muhunzi atakaepambana na Kassim Ahmad na Hashimu Chisora atazipiga na Rojas Masam uzito wa kg 61 na Julias Jackson atapambana na Emilio Norfat mpambano wa raund 4 uzito wa kg 61 na Ellsame Mbwambo atazipiga na Emanuel Kisawani mpambano wa raundi 4 uzito wa kg 61.

siku hiyo pia kutakuwa na elimu ya ujasiliamali kwa vijana wa mchezo wa masumbwi pamoja na kupatiwa mafunzo mbalimbali ya kujikwamuwa na uchumi 

Katika Mchezo huo kutakua na Uzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi pamoja na kutambua sheria zake mbalimbali zitakazokua zikisambazwa na kocha 'Super D' kwa ajili ya kuwapa mabondia mbalimbali mbinu za mchezo na mashabiki kujua sheria za masumbwi. 

Ndani yake wakiwemo mabondia Floyd Mywether, Manny Paquaio, Amiri Khani, Mohamedi Ali, Mike Tayson David Haye na wengine ambapo kutakuwa na matukio ya mazoezi yao katika mataifa yao ikumbukwe kuwa ni mabingwa wa dunia. na kutakuwa na mapambano makubwa matano ya utangulizi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad