HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, September 8, 2016

4G YA VODACOM YAKUBALIKA KWA WADAU WADAU ' HAPA KASI TU'.

 Mkazi wa Dar es Salaam, Innocent Mafuru (kushoto)  akihojiwa jana jijini na waandishi wa habari kutoka Clouds FM, Herry Mijinga kuhusiana na kasi ya intanenti ya mtandao wa kampuni hiyo unavyofanya kazi kwa kasi ya hali ya juu ukilinganisha na kipindi cha nyuma hususani tangu mtandao huo uzindue huduma ya 4G.
· Yawezesha kupakua nyimbo na picha mitandaoni fasta fasta
Kutokana na kuimarishwa zaidi kwa miundo mbinu inayotumiwa na Vodacom Tanzania kwenye huduma za intanenti kumewezesha wateja wake kufurahia huduma hii zaidi kwa matumizi mbalimbali nchini kote.

Moja ya  kundi ambalo linaendelea kufurahia matumizi  ya internet yenye kasi kubwa ni wapenzi wa muziki ambao hivi sasa wanaweza kupakua nyimbo  mitandaoni kwa kasi kubwa ikiwemo kuangalia picha za sinema kwa viwango vyenye ubora mkubwa.

Wakiongea wakati wa thathmini ya kasi na ubora wa mtandao wa Vodacom,Baadhi ya wateja walieleza kuwa hivi sasa wanaweza kupata huduma za internet kwa urahisi mahali popote na kwa wakati wowote. 

Mmoja wa wateja  Innocent Mafuru alisema kuwa akiwa mtumiaji wa mteja wa Vodacom anaweza kutumia interneti bila kupata usumbufu wowote kwa matumzi yake binafsi na matumizi yake ya  ofisini.

“Intanenti yenye kasi ya Vodacom inaniwezesha kuperuzi mitandao mbalimbali na kupakua nyaraka mbalimbali mitandaoni ikiwemo kupata  burudani za muziki na picha za sinema kutoka kwenye mitandao”.Alisema Mafuru.
Mteja mwingine Sunday John alisema kuwa interneti ya Vodacom ina kasi ya kuridhisha kwa matumizi mbalimbali ya  ofisini,kupata nyaraka kutoka mitandaoni , kutuma na kupokea nyaraka kwa kasi bila kusahau kupakua muziki na picha za sinema .

“Nimekuwa mtumiaji mzuri wa mtandao wa Vodacom na mar azote nimekuwa nikifurahia huduma zake za interneti”.Alisema.

Mtandao wa  interneti umeendea kwa asilimia 90% hivyo unawezesha idadi kubwa ya Tanzania kuufurahia kwa kupata burudani za muziki na picha kutoka mitandaoni kwa ubora na viwango vya kimataifa.
 .Mteja wa Vodacom Tanzania, Suka Keba (kushoto) akitoa maoni yake kuhusiana na kasi ya intanenti ya mtandao wa kampuni hiyo unavyofanya kazi kwa kasi ya hali ya juu ukilinganisha na kipindi cha nyuma.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad