HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, August 30, 2016

WANACHAMA CHA STDFAA WAIOMBA SERIKALI KUHARAKISHA SERA YA FILAMU.

 Katibu wa Chama hicho, Jafari Makatu (Katikati) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo. Wengine ni wasanii wa chama cha Waigizaji cha Mkoa wa Kinondoni (STDFAA).

Na Jacquiline Mrisho - MAELEZO
CHAMA cha Waigizaji cha Mkoa wa Kinondoni (STDFAA) wamemuomba Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe Nape Nnauye kuiharakisha Sera ya filamu ili iwasaidie katika mambo mbalimbali hususani ya kisheria.

Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Katibu wa Chama hicho, Jafari Makatu alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kwa ajili ya kutoa pongezi kwa Serikali ya Awamu ya Tano pamoja na kuzungumzia changamoto zinazowakabili katika tasnia ya filamu nchini.

Makatu amesema kuwa Sheria ya Filamu ni muhimu katika tasnia hiyo hivyo ikiharakishwa itasaidia wadau wa tasnia hiyo kufanya kazi kwa uwazi na usalama wa hali ya juu kwa kuwa watakua wanalindwa na sheria.

“Tunamuomba Waziri wetu Mhe. Nape atuharakishie Sera ya Filamu kwa sababu sheria hiyo itatusaidia kuoanisha mambo mbalimbali ya kisheria kuanzia kwenye uandaaji wa kazi zetu hivyo, kupelekea kufanya kazi kwa  ufanisi na kutoa kazi bora zaidi”. Alisema Makatu.

Ameongeza kuwa sheria hiyo pia itawasaidia katika suala zima la Haki miliki na Haki shiriki, malipo stahiki kwa kila kazi, masoko, madaraja ya waigizaji na wadau wote wa tasnia ya filamu pamoja na ulazima wa kila msanii kujiunga katika vyama husika vitakavyowasaidia katika mambo mbalimbali.

Aidha, Katibu huyo ameiomba Serikali kuwekeza kwenye sanaa ili kuwawezesha kuifanya kazi hiyo kwa ufanisi na kuchangia katika Pato la Taifa pia amemuomba Mhe.Nape kuwatafutia eneo maalum la ardhi ambalo litawasaidia katika kufanyia shuhuli zao za kurekodi filamu.

Ametoa rai kwa wasanii kujiunga katika vyama mbalimbali vinavyowahusu ili kuleta umoja, mshikamano na tija katika kazi za sanaa,amesisitiza wasanii kujiunga na Bima za Afya.

Naye Mdhamini wa Chama hicho, Ahmed Olotu amewaomba waandishi wa habari kutumia kalamu zao katika kuwasaidia wasanii kupambana na wauzaji  wa filamu feki kwa kuwa wanarudisha nyuma maendeleo ya wasanii na kupunguza pato la Taifa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad