HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, August 25, 2016

WABUNGE WA VYAMA VINNE WAKUBALI USHAHURI WA VIONGOZI WA DINI.

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.
VYAMA vinne vyenye uwakilishi bungeni vimesema kuwa watarejea bunge lijalo kutokana na ushauri wa viongozi wa dini waliokaa kujadili sintofahamu kwa vyama hivyo.

 Akizungumza na waandishi habari leo jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa NCCR-MAGEUZI, James Mbatia amesema viongozi wa dini wamefanya kazi kubwa katika majadiliano hayo kwa kuweka masilahi mapana ya taifa.

Amesema kuwa kurudi katika bunge lijalo mpaka wabunge wote wa vyama wakutane na kuweza kufikia mwafaka huo kutokana na ushauri wa viongozi hao.

Mbatia amesema kuwa kuna vitu vingine huwezi kuangalia katika katiba huvyo unahitaji busara zaidi kwa kuangalia masilahi mpana ya taifa.

Amesema kuwa NaibuSpika , Dk.Tulia Ackson anatakiwa kuweka busara katika kuongoza bunge na kuacha taratibu kanuni za bunge pamoja na katiba.

Aidha amesema kuwa viongozi wa dini wameshauri vyama kurejea bungeni na kutaka masuala yao wanayoyataka kikatiba yatatuliwe.
 Mwenyekiti wa NCCR-MAGEUZI, James Mbatia akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani juu ya vyama vinne vyenye uwakilishi bungeni  vitarejea bunge lijalo kutokana na ushauri wa viongozi wa dini waliokaa kujadili sintofahamu kwa vyama hivyo katika mkutano uliofanyika leo Makao Makuu ya chama NCCR -MAGEUZI jijini Dar es Salaam.
 Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Zanzibar, Said Issa Mohamed akizungumza na waandishi habari juu ya maazimio ya viongozi wa dini jana katika mkutano uliofanyika leo Makao Makuu ya chama NCCR -MAGEUZI.
Waandishi wakimsikiliza Mwenyekiti wa NCCR-MAGEUZI, James Mbatia leo Makuu ya chama NCCR -MAGEUZI jijini Dar es Salaam.
(Picha na Emmanuel Massaka, Globu ya Jamii.)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad