HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, August 26, 2016

MSHINDI WA TUZO NA MWANAMUZIKI MACHACHARI KUTOKA NCHINI NIGERIA 'YCEE ' KUKONGA NYOYO ZA WATANZANIA KATIKA ZIARA YAKE BARANI AFRIKA

YCEE ambaye pia hufahamika kwa jina la Oludemilade Martin Alejo, anatarajiwa kufika jijini Dar es salaam tarehe 28th Agosti 2016 , ikiwa ni sehemu ya ziara yake yenye lengo la kutangaza nyimbo zake ambazo ni Omo Alhaji, Jagabana' na nyinginezo. Ziara hiyo itaambatana na mkutano wa waandishi wa habari siku ya Jumatatu tarehe 29th Agosti 2016, ikifuatiwa na ziara ya kutembelea vituo mbalimbali vya habari kuanzia tarehe 29th Agosti 2016 mpaka tarehe 1 Septemba 2016.

Msanii huyo aliyepata umaarufu kupitia wimbo wa ' Jagaban ' na ' Omo Alhaji ' amedhamiria kuungana na mashabiki, wazalishaji wa muziki na wasanii mbalimbali hapa nchini  ili waweze kujenga mahusiano imara zaidi.

Pamoja na hayo amesema kuwa, anayo shahuku kubwa juu ya ziara yake kwani hii ni mara yake ya kwanza hapa nchini."Nina hamu sana ya kukutana na mashabiki wangu wa Tanzania, kwa sababu upendo wanaonipa kupitia mitandao ya kijamii ni wa ajabu na nina furaha sana ya kukutana na watu wapya " , alisema.

 
Baada ya ziara yake nchini Tanzania , YCEE ataenda nchini South Africa kuendelea na ziara yake yakukuza na kutangaza muziki wake, na anatarajia kuachia orodha ya nyimbo mpya baadaye mwaka huu utakao fahamika kwa jina la ‘The First Wave'.

Msanii huyo wa Omo Alhaji 'YCEE' pia ni miongoni mwa wasanii wanaopenda kusaidia jamii kwa kuwafikia vijana wa kiafrika katika masuala ya maendeleo na michezo.

Hivyo katika ziara yake hapa nchini YCEE atatoa msaada wa fedha kwa kituo cha masuala ya umaskini na ukosefu wa upatikanaji wa elimu kwa watoto wa mitaani Kigamboni. Kigamboni Community Center (KCC) , ni kituo kinacho shughulika na masuala ya kutokomeza umaskini, huku kikijikita katika kutoa elimu ya chekechea na msingi kwa watoto ambao wako mbali na upatikanaji wa elimu. KCC pia hutoa fursa nyingine za kujifunza kwa vijana wa Kigamboni, na pia hutoa elimu ya jamii, madarasa ya kuendeleza vipaji na mafunzo ya ufundi stadi. YCEE ameamua kuunga mkono kituo hiki kwa kwa sababu ya kujitolea kwao kukuza vipaji na kujenga upatikanaji wa elimu kwa jamii.

LINKI ZA KUSIKILIZA NA KUTIZAMA NYIMBO ZAKE

Download link for Jagaban (Audio)

http://bit.ly/2bbKpff

Download link for Jagaban (Video)

http://bit.ly/1ia65Hl

Download link for Su Mi (Audio)

http://bit.ly/2b9IAR3

Download link for Su MI (Video)

http://bit.ly/2bIOjcy

Download link for Omo Alhaji  (Audio)

http://bit.ly/2bYViCn

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad