HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, August 28, 2016

MKUU WA MKOA WA MWANZA ATEMBELEA MFUKO WA PENSENI WA PPF KANDA YA ZIWA

Mkuu wa Mwanza, John Mongella akisalimiana na baadhi ya wafanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Kanda ya Ziwa, wakati alipofanya ziara yake ya kwanza ya kutembelea ofisi za taasisi mbalimbali za umma jijini humo.
Meneja wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Kanda ya Ziwa, Meshach Bandawe akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, namna Mfuko huo unavyofanya kazi, ambapo alisema kuwa mfuko huo sasa unawalipa mafao wanachama wake kwa wakati ambapo umevuka lengo kwa kukusanya michango ya shilingi bilioni 17.03  kati ya shilingi bilioni 17.6 za lengo kwa mwaka jana ulioishia juni 2016. Bandawe alimweleza mkuu huyo wa mkoa kuwa mfuko wa PPF umefanikiwa kusajili wanachama wapya 13,028 kwa Kanda ya Ziwa pekee ikiwa ni sawa na asilimia 105 ya lengo la kusajili wanachama 12,350 kwa kipindi cha mpaka juni 2016.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella akiangalia Kadi yake ya Uanachama wa PPF aliyokabidhiwa na Meneja wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Kanda ya Ziwa, Meshach Bandawe.
Meneja wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Kanda ya Ziwa, Meshach Bandawe akimkabidhi Kadi ya Uanachama wa PPF, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, DCP Ahmed Msangi.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella akipatiwa maelezo na Meneja wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Kanda ya Ziwa, Meshach Bandawe (shati jeupe) wakati alipotembelea moja ya Idara ya Mfuko huo, Jijini Mwanza.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella akiendelea na ziara yake maeneo mbalimbali ya Mfuko huo.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, akiongozana na Meneja wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Kanda ya Ziwa, Meshach Bandawe kutembelea maeneo mbalimbali ya Mfuko wa Pensheni wa PPF, Kanda ya Ziwa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad