HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, August 29, 2016

MECHI YA YANGA NA JKT RUVU YAPIGWA KALENDA

BODI ya Ligi Kuu (TPLB) ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imethibitisha kuwa mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Young Africans ya Dar es Salaam na JKT Ruvu ya Pwani, uliopangwa kufanyika Jumatano Agosti 31 mwaka huu kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam imeahirishwa mpaka itakapopangiwa tarehe nyingine.

Mabadiliko hayo hayatavuruga ratiba ya mechi zinazofuata za Ligi Kuu ya Vodacom kwa timu husika.

Taarifa hiyo imekuja baada ya uongozi wa Yanga kutuma barua ya kuomba kusogezwa mbele kutokana na idadi kubwa ya wachezaji wake kujiunga na timu zao za taifa na tayari Yanga na JKT Ruvu wameshapatiwa barua za kujulishwa.

TFF imesogeza mbele mchezo huo, na utapangwa tena lini utachezwa, ligi itaendelea Septemba tatu mwaka huu kwa michezo minne kupigwa kwenye viwanja tofauti.

Mbao FC  wataikaribisha Mbeya City katika Uwanja wa CCM Kirumba, Kagera Sugar watakuwa kwenye uwanja wao wa nyumbani wa Kaitaba kuialika Mwadui FC, Majimaji FC watawakaribisha Mtibwa Sugar kwenye dimba la Majimaji Songea huku JKT Ruvu wakiumana na African Lyon katika uwanja wa Mlandizi. Na Zainab Nyamka

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad