Mshambuliaji
wa Timu ya Simba, Jamal Mnyate akitafuta mbinu ya kumtoka Beki wa timu
ya JKT RUVU, Rahim Juma, ikiwa ni muendelezo michezo ya Ligi kuu
Tanzania Bara, uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar
es salaam. hadi mwamuzi wa mchezo huo, Selemani Kinugani anapiliza
kipenga cha kuashiria kumalizika kwa mchezo huo, hakuna timu hata moja
iliyoliona lango la mwenzake (0-0) na kuzifanya timu hizo kugawana point
moja moja.
Mshambuliaji wa Timu ya JKT RUVU, Saady Kipanga akiruka juubaada ya Mlinda mlango wa Timu ya Simba, Vincent Angban alipoutokea mpira huo.
KOCHA msaidizi wa Simba Jackson Mayanja amesema kuwa kikosi chake kilicheza vizuri sema mapungufu katika safu ya ushambuliaji yameinyima ushindi timu yake.
Simba imelazimishwa suluhu ya kutokufungana na JKT Ruvu katika mchezo uliochezwa kwenye dimba la Uwanja wa Taifa.
Akizungumza baada ya kumalizika kwa mchezo huo, Mayanja amesema kuwa bado wanajipanga kuweza kuhakikisha wanashinda kwenye michezo yao inayofuata.
Katika mchezo wa awali Simba walitoka na ushindi wa goli 3-1 dhidi ya Ndanda na baada ya matokeo haya wanasalia na alama nne huku kwenye michezo mingine Azam amefanikiwa kushinda 3-0 dhidi ya Majimaji ya Songea mchezo ulipigwa uwanja wa Chamazi.
Mtibwa Sugar nayo imefanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 2-1 dhidi ya Ndanda huku Mwadui Fc wakitoka kifua mbele kwa ushindi wa goli 1-0, huko Mkoani Mbeya Tanzania Prisons imetoka sare ya bao 1-1 na Ruvu Shooting, wakati huko Kaitaba Mjini Bukoba, Kagera naye kashindwa kutamba uwanja wa Nyumbani kwa kutoka suluhu ya bila kufungana na Stand United.
Mtibwa Sugar nayo imefanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 2-1 dhidi ya Ndanda huku Mwadui Fc wakitoka kifua mbele kwa ushindi wa goli 1-0.
Mtibwa Sugar nayo imefanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 2-1 dhidi ya Ndanda huku Mwadui Fc wakitoka kifua mbele kwa ushindi wa goli 1-0.
No comments:
Post a Comment