HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, July 8, 2016

MKUU WA MKOA WA MBEYA AZINDUA KIVUKO CHA KITEPUTEPU WILAYANI RUNGWE NA KUWATAKA WANANCHI KUKITUNZA KITEPUTEPU HICHO..

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya  Mh.Amos Makalla amezindua Kivuko cha Kiteputepu kijiji cha Mbaka Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya baada wananchi hao kupata shida ya kuvuka na kuhatarisha maisha kwa Kuvusha Watoto kwenda Shule kwa Kuogelea, kukosa huduma za Jamiii hasa Mto unapojaa Maji 

Tarehe 10 Juni Mhe Jenista Mhagama,Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu kitengo cha Maafa alifika kujionea changamoto hiyo na Ofisi yake ilichangia shilingi Milioni 10 na mnamo Tarehe 16 Juni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na Halmashauri alipatikana Mkandarasi na alimpa Wiki 2 amalize Kazi na akahaidi Tarehe 8 Julai Kuwa tayari  na ahadi hiyo ameitimiza.

Gharama ya Ujenzi wa Kivuko ni Shilingi Milioni 58 na kufuatia Uzinduzi huo Wakazi wapatao 700 wa Kitongoji cha Kibundungulu wameanza kukitumia Kivuko hicho kwa kupita kwa Miguu na Pikipiki

Amewataka kukitunza Kivuko hicho kwani Ujenzi wa Daraja la kudumu unahitaji Fedha nyingi zaidi ya Bilioni 1.5 hivyo ni vema wakakitunza kivuko hicho kwasasa kwani kwa kiasi kikubwa kitapunguza tatizo la kuvuka na kwenda Vijiji vingine

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mh.Amos Makalla akizungumza na wakazi wa kijiji cha Mbaka Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya katika hafra ya uzinduzi wa Kivuko cha Kiteputepu.
Muonekano wa kivuko hicho kwa juu.
Baadhi ya wacheza ngoma wa kijiji cha Mbaka Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya wakitoa burudani.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad