Makamu wa Rais Mwandamizi wa Mfuko wa Abbott (Abbott Fund) Bi.Elaine Leavenworth (kulia) akimweleza Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla (kushoto) juu ya namna Mfuko wa Abbott ulivyojipanga kuendelea kutekeleza Program mbalimbali nchini Tanzania zikiwemo za Matumizi ya Teknolojia ya kisasa katika utoaji wa Tiba, maabara za kisasa, dawa na vifaa vya mafunzo kwa wanafunzi wa masomo ya Sayansi.
Ujumbe wa viongozi wa mfuko wa Abbott (Abbott Fund) kutoka Marekani ukimsikiliza Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla mara baada ya kumtembelea Ofisini kwake leo.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia) akizungumza na viongozi wa mfuko
wa Abbott (Abbott Fund) kutoka Marekani na Tanzania waliomtembelea
Ofisini kwake jijini Dar es salaam leo kuzungumzia masuala mbalimbali ya
uboreshaji wa huduma za Afya na Elimu kupitia program mbalimbali
zinazofanywa na Mfuko huo nchini. Kutoka Kulia ni Makamu Mtendaji wa
Rais wa Mfuko wa Abbott, Stephen Fussell na Makamu wa Rais Mwandamizi wa
Mfuko wa Abbott (Abbott Fund Bi.Elaine Leavenworth (katikati).
PICHA/ Aron Msigwa –MAELEZO.
No comments:
Post a Comment