HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, May 31, 2016

TAKWIMU ZA LISHE: WATOTO 2.7 WAMEDUMAA KUTOKANA KUKOSA LISHE BORA.


 Baadhi ya Vyakula Lishe ambavyo vinatakiwa kwa kila mlo ambavyo vinatakiwa kila mtu anapokula.
Mkurugenzi wa Jukwaa la Lishe Tanzania (Panita), Tumaini Mikindo akizungumza na viongozi wa dini jijini Dar es Salaam leo kuhusiana na Lishe nchini.
 Mchungaji wa makanisa ya Kipentekoste, Sixtus Mallya akichangia mada hasa kwenye imani za dini kukataza baadhi ya vyakula na kusema kuwa vyakula hivyo vimekatazwa na Biblia amesema kuwa lishe ni kitu cha mhimu kwa ukuaji wa mwili.

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
WATOTO milioni 2.7  sawa na asilimia 35   wana udumavu kutokana na kukosa lishe hali inayofanya  serikali kupoteza pato la taifa  katika kuhudumia watoto hao.

Utadumavu huo umepungua kutoka asilimia 42  mwaka 2010 hadi kufikia asilimia 35  mwaka 2015.

Akizungumza katika mkutano wa viongozi wa dini katika suala lishe, Mkurugenzi wa Jukwaa la Lishe Tanzania (Panita), Tumaini Mikindo amesema viongozi wa dini wana umuhimu kuwa mabalozi wa kuhamasisha lishe katika ngazi ya familia katika nyumba za ibada.

Amesema kuwa  kiwango cha watoto waliodumaa hawawezi kurekebishika kutokana na kuadhiri maumbile ya mtoto pamoja na kinga yake kuwa  duni kwa ugonjwa wa utapiamlo.

Mikindo amesema kuwa suala la lishe haliangaliwi huku likiwa linaadhiri maendeleo ya familia kutokana na malezi ya mtoto aliyedumaa ni tofauti na mtoto asiyedumaa.

Nae Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Pazi Mwinyumvua amesema kuwa wanawake wanashindwa kunyonyesha watoto kwa sababu kulinda maumbile kwani mwanamke akinyonyesha kuwa maziwa yanaanguka.

Mwinyimvua amesema wanashindwa kula chakula na mbogamboga kwa madai kula mboga mboga ni suala la watu wenye kipato cha chini.



kusababisha ukuaji wao.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad