HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, May 5, 2016

SNURA AOMBA MSAMAHA KWA KUCHEZA VIDEO YA CHURA.

Msanii Wa Bongo Fleva, Snura Mushi (Snura) amewaomba radhi watanzania kwaujumla pamoja na vyombo vya serikali vinavyosimamia sekta ya sanaa kwa kutokufuata sheria, kanuni na taratibu zilizopo katika uendeshaji wa sanaa.

Ameyasema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, radhi hiyo imekuja mara baada ya Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo jana kufungia video ya wimbo wa msanii huyo wa Chura ikiwa ni pamoja na kutoonyeshwa kwenye Televisheni pamoja na kupigwa kwenye redio. Amesema kuwa tayari  video ya wimbo huo ameshatoa kwenye mtandao wa kijamii wa Youtube.
Msanii Wa Bongo Fleva, Snura Mushi (Snura) awaomba radhi watanzania kwa kufanya video isiyo na maadili ya kitanzania ya wimbo wake wa Chura ameomba radhi watanzania mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.
Meneja wa msanii Wa Bongo Fleva, Snura Mushi (Snura), Hemed Kavu akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo na kuwaomba radhi wa tanzania kwa video ya wimbo wa Msanii Snura na wimbo wake wa Chura.

Kulia ni Msanii Wa Bongo Fleva, Snura Mushi (Snura) na Kushoto ni meneja wa msanii huyo, Hemed Kavu.
Snura amesema kuwa yupo tayari kufanya upya video ya Wimbo wake wa chura ambayo itafuata maadili ya kitanzania kwani tayari ameshachukua vibali vya kufanya upya video ya wimbo huo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad