HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, April 18, 2016

KIJANA YUNUS MTOPA ANDOKA NA KITITA CHA DOLA ELFU 5 ZA STATOIL TANZANIA

Mshindi wa Shindano la Mashujaa wa Kesho lilihusisha vijana wenye umri kati ya miaka 18 na 25 kutoka mikoa ya Mtwara na Lindi, Yunus Omary Mtopa, akionekana ni mwenye furaha sana baada ya kujinyakulia kitita cha dola elfu 5, kwa kuonekana wazo lake la Biashara ya Miwa kuwa bora zaidi ya wenzake. Hafla ya shindano hilo ilifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita, katika Hoteli ya Hyatt Regency, Jijini Dar es salaam.

Mwaka huu shindano hili lilivutia vijana zaidi ya 400 ambao waliwasilisha mawazo ya biashara zao zinazolenga sekta mbalimbali za uchumi kama kilimo, ufugaji, mawasiliano, na biashara nyingine ndogondogo. Vijana waliruhusiwa kushiriki mmoja mmoja au hata kuunda vikundi vya watu wawili mpaka watatu.
Jaji Mkuu katika Shindano la Mashujaa wa Kesho lilihusisha vijana wenye umri kati ya miaka 18 na 25 kutoka mikoa ya Mtwara na Lindi, Dkt. Neema Muro, akitoa maelezo mafupi ya washiriki wa shindano hilo kabla ya kumtangaza mshindi.
Sehemu ya Wageni mbali mbali waliohudhulia hafla hiyo, wakiwa makini kumsikiliza jina la Mshindi wa Shindano la Mashujaa wa Kesho lilihusisha vijana wenye umri kati ya miaka 18 na 25 kutoka mikoa ya Mtwara na Lindi, katika hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita, katika Hoteli ya Hyatt Regency, Jijini Dar es salaam.
Mgeni rasmi katika Hafla ya kumtangaza Mshindi wa Shindano la Mashujaa wa Kesho lilihusisha vijana wenye umri kati ya miaka 18 na 25 kutoka mikoa ya Mtwara na Lindi, Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Bengi Issa, akikabidhi mfano wa hundi kwa Mshindi wa Shindano hilo, Yunus Omary Mtopa.
Mgeni rasmi katika Hafla ya kumtangaza Mshindi wa Shindano la Mashujaa wa Kesho lilihusisha vijana wenye umri kati ya miaka 18 na 25 kutoka mikoa ya Mtwara na Lindi, Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Bengi Issa (wa nne kulia), Balozi wa Norway nchini Tanzania, Hanna-Marie Kaarstad (wa pili kushoto), Meneja Mkazi wa Kampuni ya Statoil Tanzania, Øystein Michelsen (shoto) wakiwa katika picha na washiriki wa shindano hilo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad