HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, February 11, 2016

MKUU WA MKOA WA DODOMA CHIKU GALAWA APOKEA MSAADA WA VITU MBALIMBALI KUTOKA VODACOM FOUNDATION KWA NIABA YA UONGOZI WA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA HUO.

 Meneja Mauzo wa Vodacom Tanzania Kanda ya Kati, Balikulije Mchome(wakwanza kushoto)akisaidia kutandika shuka katika wodi ya Watoto hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma mara baada ya kukabidhi msaada wa mashuka na magodoro pamoja na vitu mbalimbali jana ktoka Vodacom Foundation wenye thamani ya zaidi shilimgi milioni 18,Katikati Doris Mollel mwanzilishi wa taasisi ya kusaidia watoto ya Doris Foundation,na Mkuu wa Idara ya watoto ya hospitali hiyo Dkt.David Mzava.
 Mganga Mfawidhi hospitali ya Rufaa ya Dodoma Dkt. Zainabu Chaula (kushoto)akikabidhiwa msaada wa mashuka na Mkuu wa Vodacom Tanzania Kanda ya Kati,Mruta Hamisi jana kwa ajili ya wodi ya watoto hospitalini hapo,Vodacom Foundation ilitoa msaada wa mashuka 200,mito 200 na magodoro 100 vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya sh milioni 18.
 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Chiku Galawa (katikati) akikabidhiwa msaada wa magodoro 100 na Mkuu wa Vodacom Tanzania Kanda ya Kati,Mruta Hamisi (kushoto)Jumla ya magodoro 100 ,mashuka 200 na mito 200 vyote vyenye thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 18 vilitolewa msaada na Vodacom Foundation hospitalini hapo kwa ajili ya wodi ya watoto, Anayeshuhudia kulia Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo Dkt. Zainabu Chaula.

 Mganga Mfawidhi hospitali ya Rufaa ya Dodoma Dkt. Zainabu Chaula (kushoto)akikabidhiwa msaada wa muto wa kulalia na Mkuu wa Vodacom Tanzania Kanda ya Kati,Mruta Hamisi jana kwa ajili ya wodi ya watoto hospitalini hapo,Vodacom Foundation ilitoa msaada wa mashuka 200,mito 200 na magodoro 100 vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya sh milioni 18 .Katikati Doris Mollel mwanzilishi wa taasisi ya kusaidia watoto ya Doris Foundation.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad