HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, October 10, 2015

BENKI YA CRDB YASAIDIA UJENZI VYUMBA VYA MADARASA GEITA

Benki ya CRDB kupitia tawi lake la mjini Geita imechangia ujenzi wa vyumba vya madarasa katika  Shule za Msingi Mwatulole na Shule ya Msingi Geita ambayo baadhi ya majengo yalibomolewa na mvua kubwa iliyoambata na upepo mkali mwanzoni mwa mwake huu mkoani Geita. 

Sambamba na kusaidia ujenzi na ukarabati wa madarasa Benki ya crdb ilichangia maadhimisho ya wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani yaliyofanyika mjini Geita kwa sababu benki hiyo inawajali wateja wake. Maadhimisho ya wiki Huduma kwa Wateja ilianza Oktoba 5 na kumalizika Oktoba 10 ambapo Benki ya CRDB ilishiriki kikamilifu katika kazi za kijamii. Benki ya CRDB imewashuru wateja wake kupitia tawi la Geita.
Meneja wa CRDB Geita, Amini Mwakang'ata (kushoto) akimkabidhi hundi ya shilingi milioni moja Mkuu wa Shule ya Msingi Mwatulole iliyopo Mkoani Geita, Catherine Mugusi  kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja.
Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Mwatulole akipokea msaada wa vitabu vya ziada na kiada kutoka kwa Meneja wa CRDB Geita, Amini Mwakang'ata.
Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Mwatulole akipokea msaada wa vitabu vya ziada na kiada kutoka kwa Meneja wa CRDB Geita, Amini Mwakang'ata.
Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Mwatulole akipokea msaada wa vitabu vya ziada na kiada kutoka kwa Meneja wa CRDB Geita, Amini Mwakang'ata.

Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa Benki ya CRDB, Willy Kamwela (kushoto) akipokea maoni kutoka kwa mteja wa wa Benki ya CRDB tawi la Geita wakati wa Maadhiisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja mjini Geita.
Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa Benki ya CRDB, Willy Kamwela akizungumza na wateja wa benki hiyo (hayupo pichani) katika maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja iliyofanyika katika tawi la Geita.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad