HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, September 4, 2015

SERIKALI YA AWAMU YA TANO YAOMBWA KUREKEBISHA ADHABU YA KIFO

Kushoto ni Mkurugenzi wa Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wajane na kusaidia watoto,Utti Mwang’amba akizungumza na waandishi habari juu ya  serikali ya awamu ya tano kurekebisha sheria ya kifo kwa makundi maalum iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam, Pamoja na wajumbe waliohudhuria katika mkutano huo.
Waandishi wa habari wakifatilia taarifa katika ukumbi wa idara ya habari Maelezo  leo jijini Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda ,Globu ya Jamii
TAASISI  ya Children Education Society (CHESO) imeitaka serikali ya awamu ya tano kurekebisha sheria ya adhabu ya kifo  ili kulinda makundi maalum wakiwamo watoto na akina mama wajawazito.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar Es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo, Richard Shilamba amesema Serikali ya awamu ya tano wanaiomba kuondoa adhabu ya kifo katika makundi maalum kutokana na kuwa na mahitaji maalumu.

Amesema makundi hayo wakiwemo akina mama wanaonyonyesha watoto, watu wenye ugonjwa wa akili, pamoja na wazee na badala yake watafutiwe adhabu nyingine.

Shilamba amesema nchi mbalimbali ikiwemo Marekani zimeweza kufuta sheria ya adhabu ya kifo katika makundi maalum na kufanya hivyo hakujaweza kuadhiri masuala yote ya sheria.

Nae Mkurugenzi wa Kituo cha Msaada wa Sheria kwa wajane na kusaidia watoto,Utti Mwang’amba amesema wanawake wajawazito akifungwa na kutambua maisha yake ni kifo kinaweza kuadhiri ujauzito wake hivyo kwa wanawake wa jamii hiyo wanaweza kubadilisha adhabu nyingine na sio ya kutumikia kifungo kisicho na ukomo.

Katibu Mtendaji wa Kisarawe  wa Taasisi Paralegals Organisation, Halima Sasi amesema kuna wajibu wa kuangalia sheria ya watoto, makosa yenye adhabu ya kifo.

Halima ameiomba serikali ya awamu ya tano kurekebisha sheria kuangalia sheria ya kumuwezesha mtoto wa makosa ya mauaji kesi yake kuendeshwa katika mahakama za watoto .

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad