HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, August 28, 2015

ADHA YA MBWENI JKT, MANISPAA YA KINONDONI

Ukiwa na haraka Mbweni JKT jiandae kupiga mbizi

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
UPIGE mbizi,Ndivyo unavyoweza kusema msemo huu kama unahitaji kupita haraka haraka katika eneo la Mbweni JKT, wilayani Kinondoni, jijini Dar es Salaam, mahala panapojengwa daraja la kuvukia watu kwa miaka mitatu sasa, halina dalili za kukamilika hivi karibuni.

 Ni eneo tata,Ni eneo linalokera na kusumbua watu mno, Mbaya zaidi, ni eneo lililozunguukwa na majumba ya watu wenye ukwasi au ukubwa wa majina ya viongozi waliojenga katika eneo hilo. Eneo linalojengwa daraja hilo ni kwenye mkondo wa maji unaotokea baharini.
Gari likivuka eneo la mkondo wa bahari, ambapo pia ndipo panapojengwa daraja hilo hatua chache mkono wa kulia kutoka gari linapopita, Maji yakijaa hapo hakuna kupita wala kuvuka.


Kwa wanaofahamu tabia za mkondo huu wa bahari watakuwa wanaelewa, Na wasiofahamu ni kwamba, linakuwa na tabia za kujaa maji na kupungua kila wakati. Kwa mfano, mtu anaweza kupita saa tatu asubuhi akakuta hakuna maji mengi. Lakini dakika kadhaa mbele, maji mengi yanajaa kutokea baharini. Ukifanya makosa na  ukiwa na haraka ya kuendelea na shughuli zako, ndipo hapo unapopaswa upige mbizi.

Hapa ndipo panapojengwa daraja hili.

Itabidi uyavulie maji nguo ndipo upite, Na ikiwa unagari, huna budi kusubiri kwanza yapungue kama si kuisha kabisa maji hayo.

 Au utafute njia nyingine za kukufikisha eneo unaloelekea, ingawa njia hiyo inausumbufu mkubwa wa muda na gharama nyingine pia. Ni kutokana na hilo, serikali kwa kupitia Halmashauri ya Wilaya Kinondoni, inapaswa kuangalia kwa  jicho kuu eneo hili.

 Iangalie tatizo ni nini? Mbona daraja hilo halikamiliki kwa miaka mingi sasa, hakuna kinachoendelea, watu wanapata tabu, Mbaya zaidi ni eneo linalovutia na kusisimua, maana haiwezekani mtu kujenge nyumba kwa mamilioni ya pesa wakati njia ya kumfikisha kwake haieleweki eleweki. 

Ni wazi Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kinondoni pamoja na DC Paul Makonda wanapaswa kuliangalia suala hili kwa kina.


Kama serikali haina fedha za kukamilisha mradi huo iwachangishe wananchi wake, maana hii adha wanayokutana nayo ya kupiga mbizi si nzuri, kwani inapoteza muda, inadhalilisha pia.
 

Ikiwa mtu anasafiri nje ya nchi, anawahi uwanja wa ndege, anaweza kushindwa kusafiri kwa kuchelewa ndege yake kama atafika kwenye eneo hilo na kukuta maji yamejaa. 

Ni aibu na fedheha kubwa, mtaa umezungukwa na majumba ya mamilioni ya pesa mtaa umezaja watu wengi wenye nazo, viongozi wakubwa, lakini njia wanayopita inapitika kwa vipindi vya maji kujaa na kuisha. 

Hii haiwezekani Serikali iliangalie hili la mradi wa daraja la Mtaa Mbweni JKT, ambalo  linajengwa chini ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad