HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, July 31, 2015

TRA YAWAPIGA MSASA CTI JUU YA SHERIA MPYA YA KODI YA ONGEZEKO LA THAMANI YA MWAKA 2014

 Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Rished Bade akiongea na wadau kutoka Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) wakati wa semina ya kuwajengea uelewa kuhusu Sheria Mpya ya Kodi ya Ongezeko la Thamani ya mwaka 2014 iliyoanza kutumika kuanzia Julai 1, 2015, Leo Jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) Dkt. Samuel Nyantahe akimshukuru Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Rished Bade kwa uamuzi wa kuwakutanisha wadau wa sekta ya viwanda na kuwaelimisha kuhusu Sheria Mpya ya Kodi ya Ongezeko la Thamani ya mwaka 2014 ili kuweza kuondoa utata kwenye baadhi ya maeneo yaliyo katika sheria hiyo, Leo Jijini Dar es Salaam.
 Wadau kutoka Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wakimsikiliza Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Rished Bade wakati wa semina ya kuwajengea uelewa kuhusu Sheria Mpya ya Kodi ya Ongezeko la Thamani ya mwaka 2014 iliyoanza kutumika kuanzia Julai 1, 2015, Leo Jijini Dar es Salaam.
 
 Mkurugenzi Mtendaji wa Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) Leodger Tenga akimpongeza Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Rished Bade baada ya kumaliza kuwahutubia wajumbe kutoka Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI), leo Jijini Dar es Salaam.
 Afisa Mwandamizi Toka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Beldom Chaula akiwasilisha mada kuhusu Sheria Mpya ya Kodi ya Ongezeko la Thamani ya mwaka 2014 wakati wa semina ya kuwajengea uelewa kuhusu Sheria hiyo iliyoanza kutumika Julai 1, 2015 Leo Jijini Dar es Salaam.
 Wajumbe kutoka Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) wakiuliza maswali kwa wawakilishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuhusu Sheria Mpya ya Kodi ya Ongezeko la Thamani ya mwaka 2014.
 Makamu wa pili wa mwenyekiti kutoka Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) Bw. Pankaj Kumar akiongea wakati wa semina ya kuwajengea uelewa kuhusu Sheria Mpya ya Kodi ya Ongezeko la Thamani ya mwaka 2014 iliyoanza kutumika kuanzia Julai 1, 2015, Leo Jijini Dar es Salaam.
 Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Rished Bade akitolea ufafanuzi baadhi ya hoja zilizoibuliwa na wadau kutoka Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) kuhusu Sheria Mpya ya Kodi ya Ongezeko la Thamani ya mwaka 2014, wakati wa Semina ya kuwajengea uelewa Kuhusu Sheria Hiyo
 Afisa Kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Donasian Assey akitolea ufafanuzi baadhi ya hoja zilizoibuliwa na wadau kutoka Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) kuhusu Sheria Mpya ya Kodi ya Ongezeko la Thamani ya mwaka 2014.
  Afisa Mwandamizi Toka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Beldom Chaula akitolea ufafanuzi baadhi ya hoja zilizoibuliwa na wadau kutoka Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) kuhusu Sheria Mpya ya Kodi ya Ongezeko la Thamani ya mwaka 2014.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) Leodger Tenga akimueleza Jambo Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Rished Bade wakati wa semina ya kuwajengea uelewa kuhusu Sheria Mpya ya Kodi ya Ongezeko la Thamani ya mwaka 2014 iliyoanza kutumika kuanzia Julai 1, 2015, Leo Jijini Dar es Salaam.

Afisa Mwandamizi Toka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Beldom Chaula akiwaeleza jambo baadhi ya wadau kutoka Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) wakati wa semina ya kuwajengea uelewa kuhusu Sheria Mpya ya Kodi ya Ongezeko la Thamani ya mwaka 2014 iliyoanza kutumika kuanzia Julai 1, 2015, Leo Jijini Dar es Salaam.
PICHA NA HASSAN SILAYO -MAELEZO

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad