HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, July 31, 2015

MSHINDI WA AIRTEL TRACE NALIMI MAYUNGA KUACHIA VIDEO YA KIBAO CHAKE CHA "NICE COUPLE" KWENYE CHANEL YA TRACE LEO.


Mshindi wa shindano la Airtel Trace Music Star Nalimi Mayunga ameachia
kibao chake kipya cha " Nice Couple" video itakayorushwa kuanzia leo
katika kituo cha DSTV chanel ya Trace Urban 325

MWANZONI mwa mwezi huu, Mshindi huyo wa Airtel Trace Music star alitua
mjini Johannesburg South Afrika akitokea nchini Tanzania  ili kuanza
safari yake kujiendeleza kimuziki na kufikia ndoto zake mara baada ya
kuibuka mshindi wa mashindano makubwa yaliyoshirikisha nchi 13 barani
Afrika  yaliyofanyika tarehe 18 April 2015,

Mayunga alitangazwa mshindi na mwanamuziki wa kimataifa wa miondoko ya R& B wa nchini Marekeni , Akon and kupata zawadi nono ikiwemo deli ya


 kurekodi single ambapo mayunga alishuka nchini South Afrika  na
kuredoki nyimbo yake ya "Nice Couple" katika maeneo ya Orlando East.

Nyimbo hii tayari imeshaanza kupigwa katika vyombo na sehemu



mbalimbali nchini South Afrika.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad