HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, July 3, 2015

KAIMU KATIBU TAWALA MKOA WA RUKWA AFUNGUA RASMI MAFUNZO YA SIKU SITA YA WALIMU WAKUU NA WARATIBU ELIMU KATA

Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Ndugu Erasmus Rugarabamu akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku sita ya Walimu Wakuu Shule za Msingi na Waratibu Elimu Kata juu ya muongozo wa uendeshaji wa shule (School Management Tool Kit) pamoja na usimamizi wa ufundishaji wa kusoma, kuandika na kuhesabu leo tarehe 03 Julai 2015. Mafunzo hayo yanayoendeshwa na Serikali kupitia Wizara ya Elimu yanafanyika Mkoani Rukwa katika Chuo cha Ualimu Sumbawanga ambapo jumla ya washirikia 200 kutoka Halmashauri mbili za Manispaa ya Sumbawanga na Sumbawanga Vijijini wameshiriki kwenye awamu hii ya kwanza ya mafunzo. Mafunzo haya ni sehemu ya mpango wa BRN wenye lengo la kuinua ubora wa elimu nchini.
 Ndugu Nicholaus Moshi ambae ni Mratibu wa Programu ya Mafunzo ya Waalimu Kazini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi akizungumza katika Semina hiyo. Ndugu Moshi ni mmoja ya wawezeshaji wakuu katika Mafunzo hayo.
 Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo.
 Mkuu wa Chuo cha Ualimu Sumbawanga Bi. Witnes Maeda akitoa nasaha zake katika mafunzo hayo.
Mmoja ya washiriki akitoa neno la shukurani kwa niaba ya washiriki wote.
(Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa @Rukwareview.blogspot.com)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad