HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, July 31, 2015

FILIKUNJOMBE; MAFISADI WAMETUMA WATU WANING'OE UBUNGE NAOMBA WANANCHI WANYIMENI KURA

mbunge  wa Ludewa  Deo Filikunjombe kulia akiwa na mlemavu wa ngozi (ALBINO) mara  baada ya kumaliza mkutano wake wa kampeni za ubunge 

Na Matukiodaima Blog Ludewa
WAKATI wanachama wa chama cha mapinduzi (CCM)  kesho   wanashiriki  zoezi la kupiga kura  za maoni kuwapata  madiwani na  wagombea  watakao gombea kwa CCM ,mbunge  wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe amewashukuru wanachama wa CCM  katika jimbo hilo kwa kuonyeha  imani kubwa kwake  ukilinganisha na wagombea  wenzake  wawili na kuwa hadi  sasa anauhakika mkubwa wa kushinda tena ila ushindi utakaompa heshima ni ule wa kupata kura zote na wenzake kuambulia patupu

Filikunjombe  aliyasema hayo   wakati wa mkutano  wa kujinadi kwa  wagombea wa nafasi ya  ubunge katioka kata ya Ludewa mjini ,kuwa hadi  sasa kutokana na mapokeo  ya wananchi na  wana CCM kote walikopata kupita kwenye kata 26 za  jimbo hilo la Ludewa wamekuwa wakitamka  bayana kuwa kura  zote kwake  hivyo  kuwaomba wana CCM kwa umoja  wao kumpa moyo zaidi wa kuwatumikia tena kwa kuhakikisha  wanampatia kura  zote za ndio.

 

Alisema kwa kauli zao wagombea wenzake wawili  waliojitokeza wanaeleza bila kuficha kuwa wametumwa na watu  ambao  aliwaondoa bungeni kutokana na vitendo vyao vya ufisadi  ili  waje Ludewa  kugombea ubunge kwa ajili ya kulipa kisasi kwa kumtoa jambo ambalo hadi sasa  limegonga mwamba kutokana na wananchi na wana CCM Ludewa kuliona hilo.

"Niliifanya kazi  ile ya  kupambana na mafisadi bungeni kwa faida ya  wananchi wa Ludewa na watanzania kwa ujumla ila nashangazwa  kuona  leo wana Ludewa wachache wanakubali  kutumika na mafisadi hao kutumwa kuja kunitoa ubunge kweli ni aibu  kubwa kwa kazi kubwa ambayo mimi nimeifanya katika  jimbo la Ludewa  sikutegemea kupata mpinzani tena ndani ya chama changu.....ila naomba sana  wana Ludewa  tuungane katika vita  hii ya maendeleo na kupinga ufisadi kwa kuwanyima kura hawa "

Alisema kuwa wilaya ya  Luudewa itajengwa na wana Ludewa kwa kushirikiana na yeye kama mbunge wao na sio wale wanaotumika  kuwadanganya wananchi wa Ludewa hata kupinga kazi kubwa iliyofanyika kwa kipindi kifupi cha miaka mitano .

Filikunjombe  alisema kuwa hawezi kusema kuwa amemaliza changamoto  zote za wilaya hiyo ya Ludewa kwani kama atasema hivyo atakuwa anawadanganya  wananchi wake na kuwa pamoja na kuwa amefanya mengi ila hajamaliza changamoto  zote za jimbo la Ludewa hivyo iwapo  watampa tena nafasi hiyo ua ubunge atahakikisha anaendelea kupunguza changamoto zilizobaki.

" nimefanya kazi kubwa ya kuleta maendeleo jimbo la Ludewa ila nitakuwa nadanganya kama nitasema nimemaliza changamoto  zote pia hata wabunge  wenzangu walifanya kulingana na wakati  ule  na kila mmoja a namchango  wake katika  maendeleo ya Ludewa .....ninachowaomba wananchi mtupime  wagombea kwa kazi  tulizofanya msitupime kwa maneneo kwangu mimi ni kazi zaidi maneno kidogo"

Hata  hivyo alisema iwapo wananchi  wa kata ya  Ludewa watamchagua kuwa mbunge kwa kura za kishindo atahakikisha kero ya maji anaanza kuitatua kabla ya  serikali kuanza kufanya hivyo kwani kati ya changamoto kubwa kwa mji wa Ludewa ni pamoja na maji .

Pia  aliwataka  wananchi kupuuza  uongo unaosambazwa na wagombea hao kuwa  vikao vya juu vya chama vimepanga  kukata  jina lake  baada ya  kushindwa na kudai kuwa huo ni upotoshaji na kuwa CCm ni chama makini na hakuna mtu wa kukatwa iwapo ametekeleza sera  vema za chama.

Huku mgombea injinia Zephania Chaula akiwaomba  wananchi hao kumchagua kuwa mbunge kwani tayari ameahidiwa na  na mwenyekiti wa DP mchungaji Christopher Mtikila na aliyekuwa mbunge wa  jimbo hilo kabla ya  kuangushwa na mbunge filikunjombe mwaka 2005 Prof Raphael Mwalyosi kuwa watamsaidia  kufanya kazi pamoja .

Chaula ambae  alipingwa vikali katika mkutano huo kiasi cha kuzomewa baada ya kudai moja kati ya kazi aliyoifanya ni kuanzisha  mfereji wa umwagiliaji kata ya  Ruhuhu baada ya mkazi wa kata  hiyo aliyekuwepo mkutanoni hapo kunyosha mkono na kumpinga kuwa hakuna mradi huo ni uongo na kuwa wao  wanamtegemea mbunge wao Filikunjombe ambae amefanya mengi kwenye kata  hiyo.

Wakagti Injinia Chaula ambae  siku za hivi karibuni aliambulia kura  11 katika nafasi ya ujumbe wa NEC akipingwa  vikali mkutanoni hapo mgombea Kepten (mstaafu) Jacob Mpangala akijikuta katika wakati mgumu kufuatia mbunge Filikunjombe kuwasilisha vielelezo sahihi mbele ya viongozi wa chama na kugawa kwa wananchi hao viinavyoonyesha mgombea  huyo anavyodanganya  wananchi  kuwa alistaafu kazi wakati kuna barua ya  kufukuzwa kwake kazi kutoka TAMISEMI.

Filikunjombe alifikia hatua  hiyo ya  kukabidhi  ushahidi huo kwa chama baada ya kauli ya  vitisho ya mgombea  huyo Mpangala kumtaka aonyeshe hadharani ushahidi unaoonyesha kufukuzwa kakwe kazi kabla ya kuchukua hatua .

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad