HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, July 31, 2015

BREAKING NEWSSSS !!!!!!! KESI YA IPTL DHIDI YA KAFULILA YATUPWA NJE.

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imetupilia mbali kesi namba 301 iliyofunguliwa na Kampuni ya kufua Umeme ya IPTL, PAP pamoja na Mkurugenzi wa Kampuni ya PAP Bw Harbinder Singh Sethi dhidi ya Mbunge wa Kigoma Kusini Mhe David Kafulila kwa madai kuwa Kafulila alichafua jina kampuni hizo na muhusika huyo kwamba walichota zaidi ya 300bn kwenye akaunt ya Tegeta escrow kinyume cha sheria na taratibu.

Katika shauri hilo, Kampuni ya IPTL,PAP na Herbinder Singh Sethi walitaka Mahakama imuamulu Mhe Kafulila alipe fidia ya 310bn kwa kuchafua jina la kampuni na mkurugenzi huyo.

Katika kesi hiyo Mhe Kafulila alikuwa akitetewa na taasisi za kisheria za Legal& Human Righ Centre pamoja na kituo cha Human Righ Deffenders.

Akitoa uamuzi huo mbele ya mawakili wa Human Right Defenders na Legal & Human Right Center wakiongozwa na wakili Mtobesya huku mawakili wa IPTL, PAP na Sethi wakiwa hawakufika mahakamani, Jaji Rosemary Teemba alisema Mahakama Kuu imejiridhisha kwamba kampuni ya IPTL, PAP na Mkurugenzi wao Harbinder Sethi hawakuwa na hoja za msingi kuthibitisha madai yao kama msingi wa kufungua kesi mahakama kuu na hivyo kwa kuzingatia hali hiyo Mahakama Kuu kanda ya Dar es salaam inatupilia mbali shauri hilo kuanzia.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad