HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, July 30, 2015

BODI YA TPDC YAKAMILISHA UKAGUZI WA MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA

Bodi ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania ikiongozwa na Mwenyekiti wake Bw. Michael Mwanda, imekamilisha ziara ya kukagua miundombinu ya kuchakata gesi asilia na bomba la gesi asilia katika Mikoa ya Lindi, Mtwara na Dar es salaam. Katika ziara hiyo Bodi ya TPDC ilipata fursa ya kujionea na kufanya ukaguzi wa hatua za mwisho za ujenzi wa miundombinu hiyo.
Moja ya kisima gesi asili kinacho endelea kufanyiwa utafiti, kilichopo kisiwa cha Songo Songo ambacho kinacho endeshwa na kampuni ya Pan Africa.

Ukaguzi huo umefanyika kwa lengo la kujiridhisha kwamba Mkandarasi aliyepewa jukumu hilo amelitekeleza kwa umahiri, kulingana na makubaliano ya mkataba, na zoezi hili linafanyika kabla mkandarasi hajakabidhi mradi huu kwa TPDC.
Meneja Msimamizi wa Mradi wa bomba la gesi asilia, Bw. Sultani Pwaga, akitoa maelezo kwa Wajumbe wa Bodi juu ya mmomonyoko wa fukwe za bahari katika eneo la Mnazi bay.

Mradi huo umetekelezwa kwa kutumia fedha za mkopo wa masharti nafuu kutoka Serikali ya Jamhuri ya watu wa China. Jumla ya gharama za ujenzi wa mradi huu kwa fedha za kigeni ni Dola za Marekani zipatazo bilioni 1.225, ambapo asilimia 95 ni mkopo na asilimia 5 ni mchango wa Serikali.

Ziara Bodi ya Wakurugenzi Shirika ilianza tarehe 25 hadi 29 Julai 2015, Bodi hiyo ilitembelea eneo la Somanga Fungu kituo cha makutano ya bomba la gesi kutoka Madimba na Songo Songo, Kiwanda cha kuchakata gesi asilia Songo Songo, Vituo vya kupokelea gesi asilia Kinyerezi na Tegeta, pamoja na eneo la Kuchakata gesi asilia Madimba na visima vya kuzalisha gesi asilia Mnazi bay.
Wajumbe wa Bodi ya TPDC wakipatiwa ufafanuzi katika kituo cha Kinyerezi jijini Dar es Salaam, katika ziara ya wajumbe wa bodi hiyo kujionea na kukagua hatua za mwisho za ujenzi wa Miundombinu ya gesi asilia.

Ukaguzi huo umefanyika kwa lengo la kujiridhisha kwamba Mkandarasi aliyepewa jukumu hilo amelitekeleza kwa umahiri, kulingana na makubaliano ya mkataba, na zoezi hili linafanyika kabla mkandarasi hajakabidhi mradi huo kwa TPDC.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad