HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, April 1, 2015

PSPF YATOA SOMO KWA WADAU WA HABARI JIJINI DAR

 Mkutugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF), Adam Mayingu akifafanua jambo wakati akizungumza na Wadau mbali mbali wa Sekta ya Habari wakati wa Semina ya siku moja ya kuelezea shunguli mbali mbali za Mfuko huo kwa Wadau hao, iliyofanyika Machi 31, 2015 kwenye Makao Makuu ya PSPF, Golden Jubilee Tower, jijini Dar es salaam.
 Sehemu ya Wadau hao wakimsikiliza kwa makini Mkutugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF), Adam Mayingu alipoelezea machache juu ya PSPF.
 Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF), Neema Muro akitoa maelezo ya Mfuko huo kwa Wadau wa Sekta ya Habari walihudhulia Semina ya siku moja, iliyofanyika Machi 31, 2015 kwenye ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya PSPF, Golden Jubilee Tower, jijini Dar es salaam.
 Mdau Othman Maulid wa Zanzinews Blob, akifatilia kwa makini mafunzo hayo.
 Meneja wa Mpango wa Hiari wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF), Mwanjaa Sembe akitoa maelezo juu ya Mpango wa kujiunga na Mfuko wa PSPF kwa hiari, ambapo wadau wote waliofika kwenye semina hiyo waliweza kuijiunga na mpango huo.
 Mwanadada Shamim Mwasha wa 8020Fashions Blog akifatilia Semina hiyo.

 Mmoja wa Wadau hao kutoka Kituo cha Redio Clouds FM, Fred Fidelis "Fredwaa" akichangia mada kwenye semina hiyo.
Afisa Uhusiano wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF), Abdul Njaidi akielekeza jambo wakati wa semina hiyo.
Mdau Le Mutuz akipata taswirazz.
Dada Asha Abbinarah wa Jamii Forums akipitia kwa umakini moja ya Vyeti vya ushindi walivyopata PSPF.
Mtunza Kumbukumbu za Wanachama wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF), Linick Nkinda akionyesha moja ya kumbukumbu wadau wa habari waliotembelea Mfuko huo kujifunza maswala mbali mbali juu ya Mfuko huo.
Mie nikiwa na Shamim Mwasha, Asha Abbinarah, Barbara Hassan na Rechel Palangyo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad