Mkuu wa wilaya ya Kilwa, Abdala Ulega amewakata watendaji na watoa
huduma wilayani humo kuhakikisha huduma muhimu za matibabu hasa dawa
zinapatina muda wote ili kuboresha huduma wilayani hapo.
Ulega ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa awamu ya pili ya kampeni ya
uhamasiahaji wananchi kujiunga na mfuko wa afya ya jamii (CHF)
inafanywa na Mfuko wa taifa wa bima ya afya katika halmashauri kumi
nchi nzima iliyozinduliwa kata ya Tingi njia nne wilayani kilwa.
Ulega amesema Serikali kupitia mfuko wa uchangiaji wa bima ya afya
(NHIF) na mfuko wa afya ya jamii (CHF) imetoa fursa kwa wamiliki wa
vituo vya matibabu na watoa huduma kutumia fedha za uchangiaji huduma
kwa ajili ya ununuzi wa dawa na vitendanishi kwa ajili ya kuboresha
huduma kwa wananchi na kwamba fedha hizo sio za kulipana posho katika
vikao.
Awali, Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa Bima ya Afya, Rehani Athumani
alimweleza Mkuu huyo wa Wilaya kuwa kampeni hiyo iliyozinduliwa
leo itafanyika katika halmashauri nyingine kumi na hivyo kufanya jumla ya
halmashauri zilizohamasishwa nchi nzima kufikia 74 katika
mwaka wa fedha wa 2014/15.
Rehani alizitaja halmashauri hizo kuwa ni Kilwa, Ruangwa, Ulanga, Korogwe na
Rufiji. Nyingine tano ambazo huduma za mfuko wa CHF zitaanzishwa na
kuhamasishwa katika kampeni hii ni Halmashauri ya Kaliua, Kakonko,
Ushetu na Itirima.
Naye mwakilishi wa Shirika lisilo la Kiserikali la Mtandao wa Mifuko
ya Afya ya Jamiii nchini (TNCHF), Kidani Mhenga aliwaahidi
wananchi wa mikoa ya Lindi na Mtwara kuendelea kushirikiana nao katika
kutatua changamoto mbalimbali ili kuboresha huduma za matibabu kupitia Mfuko wa Afya wa Jamii katika mikoa hiyo.
Aliomba ushirikiano wa
wananchi kwa ujumla kwani mafanikio ya utekelezaji wa huduma za mfuko
huo zinategemea ushiriki wa wananchi katika kuchangia na kusimamia
huduma.
Hadi tarehe 31 machi, 2015 mfuko wa afya ya jamii ulikuwa umeandikisha
jumla ya kaya 930,879 sawa na wanufaika 5,85,274.
Mkuu wa wilaya ya Kilwa, Abdallah Ulega akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Njia Nne, Kata ya Tingi wilayani Kilwa, wakati uzinduzi wa awamu ya pili ya kampeni ya
uhamasiahaji kwa wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF)
inafanywa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) katika halmashauri kumi
nchi nzima.
Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF), Rehani Athumani akielezea namna kampeni hiyo inavyofanyika katika halmashauri nyingine kumi na hivyo kufanya jumla ya
halmashauri zilizohamasishwa nchi nzima kufikia halmashauri 74 katika
mwaka wa fedha wa 2014/15, katika uzinduzi uliofanyika leo katika
Kijiji cha Njia Nne, Kata ya Tingi wilaya ya Kilwa, Mkoani Lindi.
Mkuu wa wilaya ya Kilwa, Abdallah Ulega (kushoto) akipokea sehemu ya mashuka 150 kutoka kwa Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF), Rehani Athumani(kulia) kwa ajili ya Zahanati za Wilaya ya Kilwa.
Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoa wa Lindi, Fortunata Raymond akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF), Rehani Athumani (katikati). kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Kilwa, Abdallah Ulega.
Afisa Matekelezo na Uendeshaji wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Ofisi ya Mkoa wa Lindi, Paul Marenga akiongoza shunguli nzima ya uzinduzi wa awamu ya pili ya kampeni ya
uhamasiahaji kwa wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF)
inafanywa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) katika halmashauri kumi
nchi nzima.
Mkuu wa wilaya ya Kilwa, Abdallah Ulega (kulia) akimtambulisha Kaimu Mganga Mkuu Wilaya ya Lindi, Dkt. Peter Nsanya kwa wananchi wa Kijiji cha Njia Nne, Kata ya Tingi wilayani Kilwa na kuwatakama kama wanamatatizo yeyote ya kimatibabu waweze kumuona.
Mkuu wa wilaya ya Kilwa, Abdallah Ulega akiwaeleza jambo baadhi ya Wazee wa Kijiji cha Njia Nne, Kata ya Tingi wilayani Kilwa, ambao hawakuwa na uwezo wa kujilipia gharama ya kujiunga na huduma za Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF)
inafanywa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) na kuweza kuwalipia gharama hizo.Kulia ni Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF), Rehani Athumani, anaefuata ni Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoa wa Lindi, Fortunata Raymond.
Sehemu
ya Wakazi wa Kijiji cha Njia Nne, Kata ya Tingi wilayani Kilwa
wakifatilia kwa makini uzinduzi wa awamu ya pili ya kampeni ya
uhamasiahaji kwa wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF)
inafanywa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) katika halmashauri
kumi
nchi nzima.
Sehemu ya kina Mama wakazi wa Kijiji cha Njia Nne, Kata ya Tingi wilayani Kilwa wakishindana kukuna nazi ili kujipatia fursa ya kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF)
inafanywa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).
Afisa wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Fadhil Mtitu akimpima uzito na urefu mmoja wa Wakazi wa Kijiji cha Njia Nne, Kata ya Tingi wilayani Kilwa ikiwa ni sehemu ya uzinduzi wa awamu ya pili ya kampeni ya
uhamasiahaji kwa wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF)
inafanywa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) katika halmashauri kumi
nchi nzima.
Sehemu ya Wakazi wa Kijiji cha Njia Nne, Kata ya Tingi wilayani Kilwa wakipima afya zao katika uzinduzi wa awamu ya pili ya kampeni ya
uhamasiahaji kwa wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF)
inafanywa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) katika halmashauri kumi
nchi nzima.
No comments:
Post a Comment