HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, March 6, 2015

Jeshi la Zimamoto jijini Dar latoa mafunzo ya matumizi ya Mtungi wa kuzimia moto

Sargent Damian Muheya kutoka kitengo cha habari na Elimu kwa Umma Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji akitoa maelezo ya kutumia vifaa vya kuzimia moto vya huduma yakwanza kwa watumiaji wa Kivuko cha Magogoni jijini Dar es salaam tarehe 05/03/2015,ili kuwajengea uwezo wa kukabiliana na majanga ya moto katika hatua ya awali.
Sargent Damian Muheya kutoka kitengo cha Habari na Elimu kwa Umma Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji akimuongoza mmoja wa watumiaji wa kivuko cha MV Magogoni kuzimamoto kwa kutumia mtungi wa kuzimia moto wa huduma ya kwanza tarehe 4/03/2015,ili kuwajengea uwezo wa kukabiliana na majanga ya moto katika hatua za awali.
Konstebo Godfrey Peter kutoka kitengo cha elimu kwa Umma Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji akionesha matumizi ya mtungi wa kuzimia moto unaotumia hewa ya ukaa ( carbondioxide) kwa watumiaji wa kivuko cha magogoni Jijini Dar es salaam tarehe 4 na 5 march 2015, Ili kuwajengea uwezo wa kuyakabili majanga ya moto katika hatua ya awali.
Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Konstebo Godfrey Peter kutoka kitengo cha Elimu kwa Umma Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji akionesha matumizi ya Mtungi wa kuzimia moto aina ya Unga Mkavu ( dry powder) kwa watumiaji wa kivuko cha magogoni jijini Dar es salaam,mafunzo hayo yalitolewa tarehe 04 na 05 /03/2015. Lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea wananchi uwezo wa kukabiliana na majanga ya moto katika hatua za awali.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad