HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, February 1, 2015

MAGUFULI ZIARANI MKOANI MBEYA

Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli katikati akikata utepe kuashiria ufunguzi wa barabara ya Isongole-Itumba km 9 katika Wilaya ya Ileje Mkoani Mbeya. Kulia ni Mbunge wa Ileje Mheshimiwa Aliko Kibona. Wengine ni Mkuu wa Wilaya ya Ileje Bi Rosemary Sitaki Sinyamule, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Eng. Musa Iyombe pamoja na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini TANROADS Eng. Patrick Mfugale.
Wakazi wa Ileje wakishangilia mara baada ya Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli kuahidi ujenzi wa Barabara ya Mpemba-Isongole km 58 kwa kiwango cha lami.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Magufuli akizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Ileje Bi Rosemary Sitaki Sinyamule wakati wa Ukaguzi wa daraja la mto Songwe linalounganisha Wilaya ya Ileje na nchi ya Malawi.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akipewa maelezo kuhusu ukarabati wa Daraja la mto Songwe Wilayani Ileje.
Mbunge wa Ileje Mheshimiwa Aliko Kibona akimkaribisha Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Magufuli kabla ya ukaguzi wa daraja hilo la mto Songwe.kulia ni Mkuu wa Wilaya hiyo Bi. Rosemary Sitaki Sinyamule.
Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi nchini (CRB) Eng. Consolatha Ngimbwa akizungumza kuhusu usimamizi makini wa Bodi yake kwa Makandarasi kabla ya Waziri wa Ujenzi kuhutubia mamia ya wakazi wa Ileje.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akihutubia mamia ya wakazi wa Ileje na vitongoji vyake kuhusu mradi wa ujenzi wa barabara ya Mpemba-Isongole(km 58).

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Eng. Musa Iyombe akihutubia wakazi wa Ileje.
Waziri wa Ujenzi Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akikagua mzani wa Mpemba kabla ya kukagua barabara ya Mpemba-Isongole (km 58).
Kikundi cha watoto kikitoa burudani katika Mkutano huo.Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Ujenzi

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad