Ukiona umati wa watu namna hii hasa katikati ya mji,ujue kuna jambo limetokea.
Haya hili ndilo jambo lililotokea mchana huu,hii pikipiki iliyolala chini imegonga hiyo gari kwa mbele na kuja kuangukia kwa nyuma.hapo dereva wa Bodaboda kazungukwa huku akipigwa maswali lukuki ya nini kilichomsibu mpaka akapatwa na janga hilo?
Mashuhuda wakielekeza namna mchezo ulivyokuwa mpaka Bodaboda huyo kwenda kugoga ndinga iliyokuwa ikifuata foleni katika barabara ya Azikiwe,Posta mpya jijini Dar.
Mwendesha Bodaboda huyo (alievaa kizibao) akiwa kaduwaa bila kujua cha kufanya huku wakiendelea kumsubiria mzee wa feva aje kupima ajali.halafu eti jamaa hana leseni.....!!!
Dada mwenye gari akiangalia madhara kwenye gari yake.
No comments:
Post a Comment