HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, October 20, 2014

Chibuku Super yadhamini Uhuru Marathon 2014

Mratibu wa Mbio za Uhuru Marathon,Innocent Melleck (kulia) akizungumza na waandishi wa habari katika dhifa ya kukabidhiwa hundi ya shilingi milioni sita kwaajili ya udhamini wa mbio hizo,ambapo wamedhamini mbio za km 5. kushoto ni meneja usambazaji na mauzo wa Darbrew,Fred Kazindogo.

KAMPUNI ya Bia za asili ya Darbrew (TBL) kupitia bia yake ya asili ya Chibuku super imetangaza kudhamini mashindano ya mbio ndefu za Uhuru ‘Uhuru Marathon’ kwa kiasi cha Sh.  milioni 6.

Akitangaza udhamini huo jana jijini Dar es Salaam, Meneja mauzo na usambazaji wa Darbrew Fred Kazindogo, alisema, wameona ni vyema kudhamini mbio hizo kwa sababu zina lengo la kuimarisha umoja, amani na mshikamano miongoni mwa Watanzania.

Alisema huu ni mwaka wa pili kudhamini mbio hizo ambapo mwaka jana kampuni hiyo ilitoa kiasi cha milioni 5 na zilifanyika kwa mafanikio.

Alisema kuwa baada ya kuona malengo yametimia , Darbrew iliamua kuendelea kudhamini mbio hizo zinazoshirikisha wanariadha kutoka sehemu mbalimbali ndani ya nje ya nchi.

“Baada ya mwaka jana mbio hizi kufanyika kwa mafanikio makubwa, mwaka huu Kinywaji chibuku super kimeongeza udhamini wake kwa asilimia 15% ambazo ni ongezeko la milioni 1,’’ alisema kazindogo.

Ukweli ni kwamba taifa lolote duniani linapigania kuwa na uchumi imara na pasipokuwa na amani hakuna uchumi utakaoweza kukua, hivyo Darbrew kama kampuni inayotengeza bidhaa za hapa nyumbani imeona ni muhimu kuungana na Watanzania wenzetu wote kuhakikisha kuwa mbio hizi zinafanyika katika hali ya mafanikio makubwa na kuwa za kufana zaidi.

Aliongeza kwa kuyataka makampuni mengine ya ndani na nje ya nchi kujitokeza na pia kuendelea kutoa chochote walichonacho ili kufanikisha mbio hizi zenye kubeba dhima ya Taifa letu lakini pia wajitokeze kwa wingi kushiriki mbio hizi.

Naye mratibu wa Uhuru Marathon, Innocent Melleck, aliwaomba Watanzania kujitokeza kwa wingi kushiriki mbio hizo ambazo zina nia kubwa ya kutukumbukusha wajibu wetu wa kutunza na kulinda amani, umoja na mshikamano miongoni mwetu.

Alisema zawadi kwa mshindi wa kwanza inatarajiwa kuwa Sh. 2,500,000 kwa wakimbiaji wa kilomita 21 hii ni kwa upande wa wanawake na wanaume.

Mshindi wa pili kwa mbio hizo iwe kwa upande wa wanawake au wanaume kwa kilomita 21 au ataondoka na Sh 1.500,000 wa tatu Sh 1,000,000 wanne Sh 500,000 watano apata Sh 250,000 na wa sita hadi kumi sh 100,000 kila mmoja.

Pia mwaka huu kutakuwa na zawadi za ngao za heshima kwa shule za msingi na sekondari zitakazoshiriki mbio za hizo ili kutambua ushiriki wao na tayari shule 25 zimethibitisha kushiriki mbio kwa mwaka huu.

Mbio hizi zinatarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam hapo Desemba 7, mwaka huu ambapo zitaanzia na kumalizikia katika Viwanja vya Leaders club.

Mbio hizi zipo chini ya ulezi wa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania na kwa mara nyingine tena tunatarajia Mh Rais Jakaya Kikwete kushiriki mbio hizi,

Mbio hizo zimegawanywa katika makundi makuu matatu ambayo ni kilomita 3 kwa ajili ya viongozi, kilomita 5 kwa watu wote na kilomita 21  ambazo ni maalum kwa wakimbiaji nguli.

Wadhamini wengine wa mbio hizo ni pamoja na Michuzi Media Group, Jambo Leo, Mwananchi Communication Limited, CXS Africa, Kitwe General Traders, Faza Kidevu Blog, Habari Mseto Blog, Blog ya Wananchi,TBC 1,TBC Taifa,Redio Uhuru,Clouds fm,Tindwa medical service

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad