HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, September 18, 2014

WASHINDI WA TUZO ZA HABARI ZA TANAPA WATEMBELEA KIJIJI CHA UTALII WA UTAMADUNI AFRIKA KUSINI CHA LESEDI


Mshindi wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013 Gerald Kitabu (The Guardian) akisalimiana na kijana wa Kizulu katika kijiji cha Utamaduni cha Lesedi walipotembelea ili kujifunza utalii wa kiutamaduni nchini Afrika Kusini.
Mshindi wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013 Vedasto Msungu (ITV) akisalimiana na kijana wa Kizulu katika kijiji cha Utamaduni cha Lesedi walipotembelea ili kujifunza utalii wa kiutamaduni nchini Afrika Kusini.
Washindi wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013 kutoka kulia Gerald Kitabu, David Rwenyagira na Vedasto Msungu wakifurahi pamoja na wanakijiji cha Wazulu cha Lesedi walipowatembelea ili kujifunza utamaduni wao.
Mshindi wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013 David Rwenyagira (Radio Five) akishika ngao kwa ajili ya kujikinga na adui ambao ni mojawapo ya utamaduni wa Wazulu.
Washindi wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013 wakiendelea kupata somo juu ya tamaduni mbalimbali zinaopatikana nchini Afrika Kusini.
Washindi wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013 katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Kituo cha Utamaduni cha Lesedi, Afrika Kusini.
Lugha ya Kiswahili nayo yafahamika vema Afrika Kusini kama inavyoonekana hapa katika picha iliyopigwa na Washindi wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad