HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, September 21, 2014

Asasi za kiraia zafanya matembezi huru kusisitizia tamko lao juu ya Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi

Katika kuweka msisitizo juu ya tamko lao juu ya Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi utakaofanyika huko New York-Marekani tarehe 23/09/2014, umoja wa Asasi Nne zisizo za kiserikali zinazojishughulisha na kupambana na mabadiliko ya tabianchi nchini ForumCC, CAN, YouthCAN na Oxfam Tanzania zimefanya matembezi huru kwenye eneo la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Maandamano hayo yamewahusisha pia wanafunzi wa shule za sekondari za Jitegemee, Kinyamwezi, Ilala, Chanika na Maji ya Chai.
 Picha ya pamoja ya wanafunzi na viongozi wa asasi za kiraia walioshiriki matembezi hayo huru ili kuweka msisitizo juu ya tamko juu ya Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi utakaofanyika huko New York-Marekani tarehe 23/09/2014
 Afisa Miradi wa Forum CC, Fazal Issa aliyeshika kipasa sauti akifafanua jambo kwa wanafunzi walioshiriki matembezi hayo

 Matembezi huru yakiendelea
 Msimamizi wa idara ya Habari ya YouthCAN, Dickson Daniel akizungumza na wanafunzi walioshiriki matembezi huru ya kuunga mkono na kusisitizia tamko la asasi za kiraia juu ya Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi utakaofanyika huko New York-Marekani tarehe 23/09/2014
Meneja Ushawishi wa Oxfam, Eluka Kibona akizungumza na wanafunzi walioshiriki matembezi huru ya kuunga mkono na kusisitiza tamko la asasi za kiraia kuhusu Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi utakaofanyika huko New York-Marekani Septemba 23, 2014
 Mratibu wa CAN Tanzania, Sixbert Mwanga akifafanua jambo wakati wa matembezi huru ya kuunga mkono na kusisitiza tamko la asasi za kiraia kuhusu Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi utakaofanyika huko New York-Marekani Septemba 23, 2014
 Wanafunzi wa Jitegemee katika picha ya pamoja

Mwanafunzi wa kidato cha pili shule ya sekondari Ilala, Mwanaidi Ibrahim akiimbisha wimbo wa mazingira wakati wa matembezi huru ya kuunga mkono na kusisitiza tamko la asasi za kiraia kuhusu Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi utakaofanyika huko New York-Marekani Septemba 23, 2014, pembeni yake ni Afisa Miradi wa ForumCC, Fazal Issa.Picha zote na Tabianchi Blog

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad