HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, August 1, 2014

TBL yawaleta makocha toka Barcelona,Watatoa Mafunzo kwa Makocha wa Kizalendo

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi Juliana Yassoda (Katikati) akiongea na Wanahabari (Hawapo pichani) kuhusu makocha wa Timu ya Barcelona kutoka nchini Hispania ambao wako nchini kwa ajili ya mafunzo ya makocha wa Tanzania yatakayofanyika kwa muda wa siku mbili.Wengine picha toka kulia ni Balozi wa Spain nchini Mh. Luis Manuel Ceuesta Civis, Mkurugenzi wa Masoko wa TBL,Kushila Thomas,Kocha Isaac Oriol Guerrero Hernandes,Kocha Daniel Bigas Alsina.mafunzo hayo yanatolewa kwa ushirikiano na Kampuni ya  Bia Tanzania (TBL).
Balozi wa Hispania nchini Tanzania Mh. Luis Manuel Ceuesta Civis (Kulia) akiongea na Makocha kutoka Timu ya Barcelona ya nchini Hispania katika mkutano wa Wanahabari uliofanyika jijini Dar es Salaam jana (leo), makocha hao wapo nchini kwa ajili ya kutoa mafunzo ya siku mbili kwa makocha wazalendo, wa kwanza kushoto ni Kocha Daniel Bigas Alsina na katikati ni Kocha Isaac Oriol Guerrero Hernandes
Kocha Isaac Oriol Guerrero Hernandes kutoka timu ya Barcelona ya nchini Hispania (katikati) akitoa maelezo kwa wanahabari (hawapo pichani) kuhusu mafunzo ya siku mbili watakayotoa kwa makocha 30 wakizalendo.kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana Bi. Juliana Yassoda na wa kwanza kushoto ni kocha Kocha Daniel Bigas Alsina.
Makocha wa Kizalendo 30 ambao wanatarajiwa kupewa mafunzo ya siku mbili kutoka kwa makocha wa Barcelona wakiwa katika picha ya pamoja Picha zote na Benjamin Sawe kutoka Kitengo cha Mawasiliano Serikalini WHVUM

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad