MKE wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Dorcas Membe amekitaka kituo cha kusambaza Matrekta kwa wakulima cha Kariati Matrekta kupunguza tena bei za bidhaa hizo ili kuwa kimbilio kwa wakulima.
Kauli hiyo ameitoa leo jijini Dar es Salaa wakati akizindua kituo hicho ambapo alisema ingawa bei zao zipo chini wapunguze tena ili hata mkulima wa chini aweze kumudu kununua au kukopa trekta hiyo imuwezeshe kuondokana na umasikini.
Akizungumza katika uzinduzi huo alisema anapongeza uanzishwaji wa kituo hicho kwani ni kazi inayowahusu wakulima ambao idadi yake ni takribani asilimia 80.
''Nakupongeza Mkurugenzi kwa jitihada za kuanzisha kituo hiki chenye lengo la kuwawezesha wakulima kupata matrekta na zana zake kwa fedha tasilimu au mkopo, mpango huo utawakomboa wakulima wengi kuondokana na jembe la mkono'' alisema
Mkurugenzi Mtendaji wa Kariati Matrekta, Alhaji Omary Kariati alisema jambo ambalo wanalifanya ni kuunga mkono mpango wa Kilimo Kwanza wa serikali ya awamu ya nne ya Rais Jakaya Kikwete kwa vitendo.
Aidha alisema kwa kuhakikisha wakulima wanapata dhana za kilimo hadi sasa tayari wamesambaza matrekta 80 ambapo wamekuwa wakikopesha bila ya dhamana.
''Nimeisikia mama akisema kuwa tupunguze bei na namuhakikishia hapa hapa kwamba tumepunguza tena bei trekta la milioni 23 litanunuliwa kwa shilingi milioni 20''alisema
Mbali na hayo Meneja wa Uhusiano kwa Wateja Wakubwa wa Benki ya KCB, Victor Malewo amesema wanashirikiana vema na kituo hicho hivyo wakulima wategemee mambo mengi mazuri.
Mke
wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikianmo wa Kimataifa, Mama Dorcas
Membe (katikati), akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Kituo cha
Kusambaza Matrekta cha Kariati Matractor kilichopo Kinondoni Dar es
Salaam jana. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo hicho, Omary Kariati na Meneja wa Uhusiano kwa Wateja Wakubwa wa Benki ya KCB,
Victor Malewo, ambapo wamekiwezesha kituo hicho kupata mikopo ya
kununulia matrekta hayo.
Mke wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikianmo wa Kimataifa, Mama Dorcas Membe na Mkurugenzi
Mtendaji wa Kituo cha Kusambaza Matrekta kwa Wakulima ya Kariati
Matractor , Omary Kariati wakionesha tovuti ya kituo hicho baada ya
kufungulia. Tovuti hiyo ya www.kariatimatractor.com itamsaidia mkulima
yeyote aliopo nchini kupata fomu kwa ajili ya kununua matrekta hayo.
Mke wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikianmo wa Kimataifa, Mama Dorcas Membe akisoma taarifa yake kwa wanahabari.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Kituo cha Kusambaza Matrekta kwa Wakulima ya Kariati
Matractor , Omary Kariati (kulia), akizungumza na wanahabri na wageni
waalikwa kwenye ufunguzi huo wa ofisi yake.
Watendaji katika ofisi hiyo wakimsubiri kumpokea mgeni rasmi. Kutoka kulia ni Samira Ambeyi, Endilt Manfred na Happy Msesa.
Wakulima kutoka Kijiji cha Kwadelo wilayani Kondoa Mkoani Dodoma wakiangalia mashine ya kupandia mahindi.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Kituo cha Kusambaza Matrekta kwa Wakulima ya Kariati
Matractor , Omary Kariati akimuelekeza mke wa Waziri Membe namna mashine
ya kupanda mahindi inavyofanya kazi.
Mke wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikianmo wa Kimataifa, Mama Dorcas Membe akipeana mkono na Meneja wa Uhusiano kwa Wateja Wakubwa wa Benki ya KCB, Victor Malewo.
Mke wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikianmo wa Kimataifa, Mama Dorcas Membe na Mkurugenzi
Mtendaji wa Kituo cha Kusambaza Matrekta kwa Wakulima ya Kariati
Matractor , Omary Kariati wakisoma kwa pamoja kibao cha ufunguzi wa
ofisi hiyo kikimuonesha mama Membe kufungua ofisi hiyo.Picha zote na Mdau Dotto Mwaibale wa mtandao wa
www.habari za jamii.com.
Hongera sana rafiki yangu mpenzi, Mama Dorcas Membe, kwa ufunguzi wa ofisi ya kusambaza matrekta kwa wakulima.
ReplyDelete