HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, July 24, 2014

TIB Development Bank kushirikiana na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kuendeleza fukwe za Coco Beach jijini Dar

TIB Development Bank ikishirikiana na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni imefanya upembuzi yakinifu na kutayarisha michoro kwa ajili ya kuendeleza eneo la ufukweni maarufu kama Coco Beach la jijini Dar es Salaam. 

Mradi huo ujulikanao kama Coco Beach Park utaboresha mazingira na kuongeza vivutio kwenye eneo hilo pendwa kwa wakazi wa Dar es Salaam. Mradi huu utatekelezwa kwa ushirikiano na wabia mbalimbali na utakuwa unamilikiwa na Manispaa ya Kinondoni. 

TIB Development Bank inashirikiana na Manispaa nyingine mbalimbali nchini kutekeleza miradi ya maendeleo mfano Manispaa za Kagera, Moshi, Ilala, Temeke n.k
Mwenyekiti wa Bodi ya TIB Development Bank Profesa William Lyakurwa akiwa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Mhandisi Mussa Natty wakikata utepe kuzindua mradi wa Coco Beach Park. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa TIB Development Bank Bwana Peter Noni.
Bwana Jaffar Machano kutoka TIB Development Bank akiielezea michoro ya mradi wa Coco Beach Park kwa Mwenyekiti wa Bodi ya TIB Profesa William Lyakurwa na Mkurugenzi Manispaa ya Kinondoni Mhandisi Mussa Natty
Muonekano wa Coco Beach Park itavyokuwa baada ya kumalizika mradi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad