HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, April 25, 2014

Zanzibar yajivunia kupunguza vifo vya uzazi

Mkurugenzi Mipango, Sera na Utafiti wa Wizara ya Afya Zanzibar Abdul- latif Khatib Haji akizungumza na washiriki wa mkutano wa mpango wa kuboresha Afya ya mama na mtoto katika Hoteli ya Grand Palace Malindi mjini Zanzibar.
Mwakilishi wa USAID nchini Tanzania Lisa Patel, akitoa maelezo ya mradi wa MAISHA ambao umemaliza muda wake hapa nchini.
Baadhi ya washiriki wa mkutano wa kukamilisha mradi wa MAISHA kutoka mikoa yote ya Zanzibar wakimsikiliza Mkurugenzi wa mradi huo Dk. Dunstan Bishanga (hayupo pichani), akitoa hotuba katika mkutano huo.
Mkurugenzi wa Mradi wa kuboresha Afya ya mama na mtoto Tanzania Dk. Dunstan Bishanga, akitoa hotuba katika mkutano huo.
Afisa Muuguzi wa Hospitali Kuu ya Mnazimmoja Ashura Amour Mwinyi, akitoa maelezo kwa mgeni rasmi Mkurugenzi Mipango, Sera na Utafiti wa Wizara ya Afya Zanzibar Abdullatif Khatib Haji (alievaa shati jeupe), jinsi ya kuwasaidia watoto kupumua vizuri mara baada ya kuzaliwa. Hiyo ilikuwa hafla ya kukamilika kwa mradi wa kupunguza vifo vya wajawazito na watoto vitokanavyo na uzazi – MAISHA, unaofadhiliwa na Shirika la Misaada ya Maendeleo ya Kimataia la Marekani (USAID), katika ukumbi wa Hoteli ya Grand Palace Malindi.

Mkurugenzi Mipango, Sera na Utafiti wa Wizara ya Afya Zanzibar Abdul-latif Khatib Haji (katikati waliokaa), wakiwa katika picha ya pamoja ya wafadhili wa mradi wa MAISHA na wasimamizi wa mradi huo hapa Zanzibar. Wa kwanza kulia mwenye suti nyeusi ni Mkurugenzi wa mradi wa MAISHA Tanzania Dunstan Bishanga. (PICHA NA MAKAME MSHENGA- MAELEZO ZANZIBAR).

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad