HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, April 20, 2014

Familia Kitchen Party Gala ndani ya jiji la Mwanza

Wanawake wa jiji la Mwanza wamepata nafasi ya kuongea na Mama Victor,Aunt Sadaka na Getrude Mongela katika Familia Kitchen Party Gala. Shughuli imefanyika jana Jumamosi tarehe 19,katika ukumbi wa Gold Crest Hotel.

Ukiachana na maongezi kuhusu mahusiano na masuala ya kina mama,vilevile wanawake walipata nafasi ya kupata huduma na ushauri wa Uzazi wa mpango,vipimo vya saratani/kansa ya mlango wa uzazi iliyotolewa bure na Familia kupitia PSI Tanzania.
Mtaalam wa Maswala ya saikolojia,Aunt Sadaka akitoa somo kwa Wanawake wa jiji la Mwanza wakati wa hafla ya kina mama ya Familia Kitchen Party Gala.
Sehemu ya Kina mama wa Jiji la Mwanza wakifatilia mada mbali mbali zilizokuwa zikitolewa kwenye Familia Kitchen Party Gala.
Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya,Mwasiti Almas akitoa burudani kwenye hafla hiyo.






No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad