Hizi ni chochoro ambazo wakazi hao wa milimani wanazitumia kupita huku
zikiwa zimejazana mawe ambayo kwa mujibu wawenyeji mawe hayo
yanahatarisha sana usalama wa watu wanoishi chini ya milima kwasababu
mvua zinaponyesha nyingi huwa yanaporomoka.
Kama haujaangalia vizuri unaweza kudhani
ni jengo moja refu la ghorofa lakini si hivyo ila ujenzi wa milimani
jijini Mwanza, hapa ni kwenye eneo la Kata ya Isamilo ipo ubavuni mwa
jiji hilo upande wa kaskazini. Mbali ya kuwa ni mlimani lakini si milima
hivi hivi ila ni milima yenye mawe makubwa na madogo ambapo hata ujenzi
wake ni wachangamoto nyingi sana.
Hapo ndipo kwenye soko la mtaa huo ambapo wakazi wake huenda kupata mahitaji muhimu.
Hapo bondeni kidogo kuna Shule ya Sekondari ya Daniel Ole Njolai.
Hiki ni kimoja ya aina ya vyoo
vinavyojengwa, ni mawe yaliyounganishwa na tope la udongo ambapo mvua
ikinyesha unaporomoka chini.
Lakini kando ya eneo hilo wapo wanapiga
matofali ya udongo ili kubadilisha aina hiyo ya ujenzi wa mawe ambao ni
mgumu kwa watu wasio na kipato cha kuweza kununua saruji ya kujengea.
Ukiwa juu kabisa kwenye eneo la Mtaa wa
Nyakabongo C, unaweza kuona vizuri zaidi mandhari ya Jiji la Mwanza kama
inavyoonekana pichani.
No comments:
Post a Comment